-
Balozi wa Iran UN apinga madai ya Marekani kuhusu shambulio dhidi ya kinu cha nyuklia cha UAE
May 24, 2026 03:26Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa ameyatupilia mbali madai ya Marekani kuhusu shambulio la ndege zisizo na rubani (drone) dhidi ya kinu cha kuzalisha umeme kwa nishati ya nyuklia cha Barakah nchini Falme za Kiarabu (UAE). Amesema kuwa Washington imetumia vibaya Baraza la Usalama ili kusambaza tuhuma za uongo dhidi ya Iran na mpango wake wa nyuklia wenye malengo ya amani.
-
Iran yaiambia UN: Nchi za Ghuba ya Uajemi zinapasa kutoa jibu na kulipa fidia kwa mchango wao katika vita vya Marekani na Israel
May 23, 2026 12:32Amir Saeid Iravani Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa nchi za kusini mwa Ghuba ya Uajemi na Jordan zinabeba dhima ya kuzisaidia Marekani na Israel katika uvamizi wao dhidi ya Iran.
-
UN kujenga ofisi mpya yenye thamani ya dola milioni 340 Nairobi
May 12, 2026 09:01Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amshuhudia uwekezaji mkubwa wa Umoja wa Mataifa wenye thamani ya karibu dola milioni 340 katika ofisi yake katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi.
-
UN yaonya: Hatua za Marekani zimepandisha bei ya vyakula duniani
Apr 29, 2026 10:07Msemaji wa Umoja wa Mataifa ametangaza kuwa bei za vyakula duniani zimeongezeka kufuatia hatua za Marekani katika Mlango Bahari wa Hormuz.
-
UN yalaani mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya taasisi za gesi na nishati za Iran
Mar 19, 2026 07:32Naibu Msemaji wa Umoja wa Mataifa amelaani mashambulizi ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel katika taasisi za gesi na nishati za Iran pamoja na shambulio katika kisima cha gesi cha Pars-Kusini na katika eneo la Asaluyeh.
-
Wataalamu wa haki wa UN walaani mashambulizi ya US, Israel dhidi ya Iran
Mar 14, 2026 03:29Kundi moja la wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa limelaani vikali mashambulizi na jinai zinazofanywa na Marekani na Israel dhidi ya wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Lebanon.
-
Araghchi aonya UN: Kunyamazia kimya uvamizi wa US, Israel kutashadidisha taharuki katika eneo
Mar 12, 2026 03:23Waziri wa Mambo ya Nje ya Iran amesema katika mazungumzo yake ya simu na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres kuwa, kufumbia macho au kutochukua hatua za maana mkabala wa vitendo vya kivamizi vya Marekani na Israel dhidi ya Iran kutafungua njia ya kushadidi ukosefu wa utulivu na taharuki katika eneo.
-
Iran: UN inabeba dhima ya kisheria na kimaadili ya vita haramu vya US, Israel
Mar 07, 2026 10:29Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei amejibu taarifa ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ambaye bila kulaani uvamizi na mashambulizi ya kichokozi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran, ameeleza wasiwasi wake juu ya vita hivyo kwa uchumi wa dunia.
-
UN: Wakimbizi wa Burundi walioko Tanzania wanarudi makwao kwa hiari, hawashurutishwi
Feb 27, 2026 03:27Afisa wa Uhusiano wa Nje wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR nchini Tanzania Bahia Egeh amesema, wakimbizi wa Burundi walioko nchini humo ambao wanarudi makwao, wanafanya hivyo kwa hiari wala hawashurutishwi.
-
UN yatoa wito wa msaada wa dharura kwa wakimbizi wa Burundi waliopo na wanaorudi nchini
Feb 25, 2026 03:28Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, (UNHCR) limetangaza kuwa, ufadhili endelevu na wa uhakika unahitajka ili kuendeleza ulinzi kwa wakimbizi na kusaidia urejeaji na ujumuishaji wa raia wanaorudi nchini Burundi, wakati huu ambapo kambi zinzowahifadhi zinakabiliwa na msongamano mkubwa na uhaba wa huduma muhimu.