-
UN yalaani mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya taasisi za gesi na nishati za Iran
Mar 19, 2026 11:02Naibu Msemaji wa Umoja wa Mataifa amelaani mashambulizi ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel katika taasisi za gesi na nishati za Iran pamoja na shambulio katika kisima cha gesi cha Pars-Kusini na katika eneo la Asaluyeh.
-
Wataalamu wa haki wa UN walaani mashambulizi ya US, Israel dhidi ya Iran
Mar 14, 2026 06:59Kundi moja la wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa limelaani vikali mashambulizi na jinai zinazofanywa na Marekani na Israel dhidi ya wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Lebanon.
-
Araghchi aonya UN: Kunyamazia kimya uvamizi wa US, Israel kutashadidisha taharuki katika eneo
Mar 12, 2026 06:53Waziri wa Mambo ya Nje ya Iran amesema katika mazungumzo yake ya simu na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres kuwa, kufumbia macho au kutochukua hatua za maana mkabala wa vitendo vya kivamizi vya Marekani na Israel dhidi ya Iran kutafungua njia ya kushadidi ukosefu wa utulivu na taharuki katika eneo.
-
Iran: UN inabeba dhima ya kisheria na kimaadili ya vita haramu vya US, Israel
Mar 07, 2026 13:59Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei amejibu taarifa ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ambaye bila kulaani uvamizi na mashambulizi ya kichokozi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran, ameeleza wasiwasi wake juu ya vita hivyo kwa uchumi wa dunia.
-
UN: Wakimbizi wa Burundi walioko Tanzania wanarudi makwao kwa hiari, hawashurutishwi
Feb 27, 2026 06:57Afisa wa Uhusiano wa Nje wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR nchini Tanzania Bahia Egeh amesema, wakimbizi wa Burundi walioko nchini humo ambao wanarudi makwao, wanafanya hivyo kwa hiari wala hawashurutishwi.
-
UN yatoa wito wa msaada wa dharura kwa wakimbizi wa Burundi waliopo na wanaorudi nchini
Feb 25, 2026 06:58Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, (UNHCR) limetangaza kuwa, ufadhili endelevu na wa uhakika unahitajka ili kuendeleza ulinzi kwa wakimbizi na kusaidia urejeaji na ujumuishaji wa raia wanaorudi nchini Burundi, wakati huu ambapo kambi zinzowahifadhi zinakabiliwa na msongamano mkubwa na uhaba wa huduma muhimu.
-
Ripota wa UN kuhusu Palestina asema, licha ya kuandamwa hatasalimu amri, hatajiuzulu
Feb 21, 2026 02:36Francesca Albanese, ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa wa maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu, amesema hatajiuzulu wadhifa wake huo licha ya mashinikizo yanayotolewa dhidi yake na serikali za nchi kadhaa za Ulaya kutokana na matamshi yanayodaiwa kuwa ametoa dhidi ya utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Wachunguzi wa UN: Yumkini mauaji ya halaiki yamefanyika El-Fasher
Feb 20, 2026 03:27Ujumbe wa kutafuta ukweli wa Umoja wa Mataifa umesema ukatili uliofanywa na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka RSF wakati wa kuutwaa mji wa El-Fasher huko Darfur Magharibi nchini Sudan mwezi Oktoba mwaka jana, una "alama za mauaji ya kimbari" dhidi ya jamii za Zaghawa na Fur.
-
Nchi 80 zalaani mpango wa Israel wa kughusubu Ukingo wa Magharibi
Feb 18, 2026 06:25Zaidi ya nchi 80 wanachama wa Umoja wa Mataifa zimelaani mpango wa Israel wa kupora na kuyakalia kwa mabavu maeneo kadhaa ya ardhi za Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu, na kuyatambua maeneo hayo ya Palestina kama "milki ya serikali" ya Israel.
-
Wataalamu wa UN waonya kuhusu hatari zinazowakabili waathirika wa "Mafaili ya Epstein"
Feb 18, 2026 03:05Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wamesema, wana wasiwasi mkubwa kuhusu madhara yanayoweza kuwapata waathirika waliotajwa katika nyaraka zinazojulikana kama "Mafaili ya Epstein" (Epstein Files), na kueleza kwamba mchakato wa utoaji wa taarifa hizo haukulinda ipasavyo faragha na usalama wao.