-
UN: Ujenzi wa vitongoji katika ardhi za Palestina ni haramu na inapasa usimamishwe kikamilifu
Apr 22, 2017 11:55Mratibu wa amani wa Umoja wa Mataifa amesema, kwa mujibu wa sheria za kimataifa, ujenzi wa vitongoji unaofanywa na Israel katika ardhi unazozikalia kwa mabavu za Palestina ni kinyume cha sheria na inapasa usimamishwe kikamilifu.
-
Al Jaafari: Israel na ugaidi ni pande mbili za sarafu moja
Apr 20, 2017 23:44Mwakilishi wa kudumu wa Syria katika Umoja wa Mataifa amesisitiza kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel na ugaidi ni pande mbili za sarafu moja na amemlaumu vikali Nikolay Mladenov, mratibu maalumu wa umoja huyo katika mazungumzo ya mapatano ya Mashariki ya Kati kwa kudharau kutaja milima ya Golan ya Syria inayokaliwa kwa mabavu na Israel, katika ripoti yake kwa umoja huo.
-
UN yaionya Saudia dhidi ya kushambulia kwa mabomu bandari ya Yemen
Apr 20, 2017 09:43Umoja wa Mataifa umeutaka muungano wa kijeshi wa Saudi Arabia usishambulie kwa mabomu bandari ya kistaratejia ya Yemen.
-
Ushirikiano wa kiusalama kati ya Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika
Apr 20, 2017 09:33Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika wamesaini makubaliano ya kushirikiana katika suala la usalama.
-
UN yagundua makuburi mengine 17 ya umati nchini Kongo DR
Apr 19, 2017 10:55Timu ya wachunguzi ya Umoja wa Mataifa imegundua makaburi mengine 17 ya umati katika mkoa wa Kasai, katikati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wiki mbili baada ya makaburi mengine kugunduliwa katika eneo hilo.
-
Ethiopia yakataa wito wa UN na EU wa kufanyika uchunguzi dhidi yake
Apr 18, 2017 21:59Waziri Mkuu wa Ethiopia amekataa wito wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya wa kufanyika uchunguzi huru juu ya mauaji ya mamia ya watu wakati wa maandamano ya miezi kadhaa dhidi ya serikali ya Addis Ababa nchini humo.
-
Wahajiri 9000 waokolewa katika bahari ya Mediterania mwishoni mwa wiki
Apr 18, 2017 11:05Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) limesema idadi ya wakimbizi waliookolewa katika bahari ya Mediterania wakijaribu kuelekea barani Ulaya mwishoni mwa wiki imevunja rekodi.
-
Katibu Mkuu wa UN atahadharisha kuwa Daesh wanaweza kuidhibiti tena Libya
Apr 15, 2017 00:17Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametahadharisha kuhusu hatari ya kupanuka zaidi udhibiti wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh katika maeneo mbalimbali ya Libya na hali mbaya inayotawala maeneo yanayodhibitiwa na kundi hilo.
-
UN: Kipindupindu kimeua zaidi ya watu 530 Somalia
Apr 13, 2017 23:26Umoja wa Mataifa na jumuiya za misaada ya kibinadamu zimeonya kwamba kipindupindu kinaenea kwa kasi katika maeneo yaliyoathirika na ukame nchini Somalia wakati nchi hiyo ikiendelea kunyemelewa na hatari kubwa ya baa la njaa.
-
Jumuiya za haki za binadamu: Mjumbe wa UN amefeli Yemen
Apr 13, 2017 23:02Jumuiya na mashirika ya kutetea haki za binadamu yametangaza katika mkutano uliofanyika Paris nchini Ufaransa kwamba Mjumbe Maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Yemen, Ismail Ould Sheikh ameshindwa kutekeleza majukumu yake.