-
Bachelet aitaka Misri kutengua hukumu ya vifo dhidi ya wafuasi wa Ikhwanul Muslimin
Sep 09, 2018 11:37Bi Michelle Bachelet Mkuu wa Kamisheni ya Haki za Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa leo Jumapili ameitolea mwito mahakama ya rufaa ya Misri kutengua hukumu za vifo zilizotolewa na mahakama moja nchini humo dhidi ya viongozi na wafuasi wa harakati ya Ikhwanul Muslimin.
-
Nchi za dunia zinapaswa kushirikiana na Iran katika kukabiliana na mihadarati
Sep 04, 2018 22:02Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inasema nchi zote ambazo zinafaidika na jitihada zake za kupambana na mihadarati zinapaswa kuisaidia kiufundi na kifedha.
-
UN: Hali ya raia CAR inatia wasiwasi
Sep 04, 2018 02:19Ofisi ya huduma za misada ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) imeripoti kuwa hali ya wakazi wa mji wa Alindao huko kusini mashariki mwa Jamhuri ya Afrika ya Kati ni mbaya sana kutokana na mapigano yanayoendelea baina ya makundi ya waasi katika eneo hilo.
-
Russia yaikabidhi UN ushahidi kuwa Wamagharibi wanafanya njama za kuishambulia tena Syria
Sep 01, 2018 02:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema kuwa nchi yake imeukabidhi Umoja wa Mataifa ushahidi unaothibitisha kuwa nchi za Magharibi zinafanya njama za kuishambulia tena Syria kwa madai ya uongo ya matumizi ya silaha za kemikali hata kabla ya kutumika silaha hizo.
-
Ansarullah ya Yemen yautaka Umoja wa Mataifa uwe huru katika kukabiliana na wavamizi
Aug 29, 2018 23:00Msemaji wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amekosoa utendaji wa Umoja wa Mataifa na kuitaka taasisi hiyo ya kimataifa iwe huru katika kuchukua maamuzi ya kukabiliana na hatua za kivamizi za Saudi Arabia nchini humo.
-
Qatar yakerwa na jinai za kivita zinazotendwa na Saudia nchini Yemen
Aug 29, 2018 10:25Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar amekosoa ripoti ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusiana na jinai za kivita zinazotendwa na Saudia na Imarati nchini Yemen.
-
UN yakemea vikali jinai za Saudi Arabia nchini Yemen
Aug 28, 2018 07:45Mwenyekiti wa Kamati ya Haki za Watoto ya Umoja wa Mataifa amesema kuwa mashambulizi ya kinyama yanayofanywa na Saudi Arabia na waitifaki wake yameua watoto wengi nchini Yemen.
-
Kutokuwa halali vikwazo vya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Aug 22, 2018 03:32Ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu ametahadharisha kuhusianja na kuenea vita vya kiuchumi ulimwenguni na kusema kuwa, hatua ya Marekani ya kuiwekea vikwazo tena Iran si halali kisheria, ya kidhalimu na ina madhara.
-
Ripota maalumu wa UN: Vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran si halali kisheria
Aug 21, 2018 09:58Ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu na athari hasi za uchukuaji hatua za upande mmoja amesema hatua ya Marekani ya kuiwekea vikwazo tena Iran si halali kisheria, ya kidhalimu na ina madhara.
-
Ukosoaji wa Amnesty International kwa hatua ya Marekani na Ulaya ya kuiuzia silaha Saudi Arabia na Israel
Aug 21, 2018 08:20Shirika la Msamaha Duniani la Amnesty International limeikosoa Marekani na madola ya Ulaya na kuyataka yasitishe kuiuzia silaha Saudi Arabia na utawala haramu wa Israel.