-
Mkuu wa Sera za Kigeni EU afuta safari yake Tel Aviv, ongezeko la hitilafu baina ya Ulaya na Israel
Jun 09, 2018 22:20Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amefuta safari yake ya kutembelea ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu (Israel) baada ya Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel kusema hatakutana naye katika safari hiyo.
-
Hatua mpya za Ulaya kulinda makubaliano ya JCPOA
Jun 07, 2018 05:23Sambamba na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kutangaza hatua ya kuimarisha shughuli zake za nyuklia katika fremu ya mapatano ya nyuklia na nchi sita kubwa za dunia mashuhuri kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA), nchi za Ulaya zimeongeza mashauriano na juhudi za kuyalinda yasije yakasambaratika.
-
EU: Hatua ya Iran ya kuimarisha urutubishaji urani haikiuki JCPOA
Jun 06, 2018 03:03Umoja wa Ulaya umesema tathmini yake ya mwanzo inaashiria kuwa mpango wa Iran wa kuimarisha urutubishaji urani hadi kufikia kiwango cha SWU 190,000 haukinzani na makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Umoja wa Ulaya wapiga hatua katika kulinda biashara na Iran
Jun 01, 2018 09:33Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian amesema Umoja wa Ulaya umepiga hatua katika kuyalinda mashirika ya kibiasahra ya umoja huo ili yasilengwe kwa vikwazo vya Marekani kutokana na kufanya biashara na Iran. Hata hivyo amesema hatua zilizochukuliwa bado hazitoshi.
-
Kuanza vita vya kibiashara kati ya Trump na washirika wake wakuu wa kibiashara
Jun 01, 2018 09:07Hatimaye Rais Donald Trump wa Marekani ameanza kutekeleza kivitendo vita vya kibiashara kati ya nchi hiyo na washirika wake wa Ulaya kwa kuziwekea ushuru mpya bidhaa za chuma cha pua na alumini (aluminiamu) zinazoingizwa nchini humo kutoka nje.
-
Umoja wa Ulaya: Tutayalinda mapatano ya nyuklia ya Iran licha ya Marekani kujitoa + Video
May 28, 2018 10:58Mkuu wa Sera za Kigeni za Umoja wa Ulaya amesema kuwa umoja huo umeazimia kikweli kweli kuyalinda mapatano ya nyuklia yaliyofikiwa mwaka 2015 baina ya Iran na kundi la 5+1, licha ya Marekani kujitoa katika mapatano hayo ya kimataifa.
-
Kiongozi Muadhamu: Ikiwa Ulaya itazembea, lran ina haki ya kuanzisha shughuli zake za nyuklia
May 24, 2018 00:21Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria uadui wa msingi, wa kina na endelevu wa Marekani dhidi ya mfumo wa Kiislamu na taifa la Iran na kusisitiza kwamba bila shaka Iran itaishinda tu Marekani iwapo viongozi wa Iran watatekeleza vilivyo majukumu yao.
-
Radiamali ya Ulaya kuhusiana na stratijia mpya ya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
May 23, 2018 23:38Federica Mogherini, Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya ametoa radiamali yake kupitia tovuti rasmi ya umoja huo kufuatia stratijia mpya iliyotangazwa na Mike Pompeo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani dhidi ya Iran, akitangaza kufungamana kikimilifu EU na makubaliano ya nyuklia ya Iran maaruku kwa jina la JCPOA.
-
Kansela wa Ujerumani Merkel apoteza matumaini kuhusu Marekani
May 11, 2018 03:44Kansela Angela Merkel wa Ujerumani kwa mara nyingine amesema nchi za Ulaya haziwezi kuendelea kuitegemea Marekani katika masuala ya kijeshi na kujihami. Merkel amewataka waitifaki wa Ujerumani barani Ulaya wachukue hatima ya bara hilo mikononi mwao kwani Marekani haiwezi kutegemewa tena.
-
EU yapinga hatua ya Marekani kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya Iran
May 09, 2018 21:57Umoja wa Ulaya (EU) umebainisha masikitiko yake kuhusu uamuzi wa Rais Donald wa Marekani kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya Iran yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezwaji , JCPOA, na kusisitiza kuhusu kuendelea kutekelezwa na kufungamana kikamilifu na mapatano hayo.