May 13, 2018 02:48
Harakati ya Kitaifa ya Al-Wefaq ya nchini Bahrain imesema kuwa, matamshi ya Khalid bin Ahmed Al Khalifa, Waziri wa Mambo ya Nje wa Bahrain katika kuunga mkono utawala haramu wa Kizayuni, ni ya kufedhehesha na anatakiwa kuliomba radhi taifa sambamba na kujiuzulu.