-
Kukataa utawala wa Kizayuni kushirikiana na Baraza la Haki za Binadamu la UN
Feb 19, 2022 23:22Utawala wa Kizayuni umekataa kushirikiana na Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa. Mwakilishi wa Israel katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ametangaza kuwa Tel Aviv haitashirikiana na jopokazi la uchunguzi la baraza hilo kwa ajili ya kuchunguza mashambulizi ya mwezi Mei mwaka jana ya utawala wa Kizayuni huko Ukanda wa Ghaza.
-
Syria: Hatua ya Israel ya kuwafukuza Wapalestina Sheikh Jarrah ni uhalifu wa kivita
Feb 15, 2022 09:41Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Syria imetoa wito wa kukomeshwa hatua za utawala wa Kizayuni wa Israel za kuharibu nyumba za Wapalestina na kuwafukuza katika ardhi na makazi yao.
-
Sheikh Qassim: Waislamu wakabaliane na mwenendo wa kuanzishwa uhusiano na Israel
Feb 14, 2022 04:14Kiongozi wa Waislamu wa Kishia nchini Bahrain ametoa wito wa kusimama kidete Waislamu katika kukabiliana na mwenendo wa kuanzishwa uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel.
-
Hatua ya "PLO" ya kusimamisha ushirikiano wa kiusalama na utawala wa Israel
Feb 11, 2022 23:02Baraza Kuu la Harakati ya Ukombozi wa Palestina (PLO) imetangaza kusimamisha kuutambua rasmi utawala wa Kizayuni wa Israel na ushirikiano wa kiusalama na utawala huo. Baraza Kuu la PLO pia limetangaza kuwa, limesimamisha uratibu wowote wa kiusalama na utawala wa Kizayuni kwa njia mbalimbali.
-
Jihadul Islami: Mapambano dhidi ya utawala dhalimu wa Israel yataendelea kote Palestina
Feb 11, 2022 03:58Ziyad al-Nakhalah, Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Jihadul Islami amesisitiza kuwa, mapambano na muqawama dhidi ya utawala vamizi wa Kizayuni wa Israel yataendelea katika maeneo yote ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.
-
Radiamali kwa hatua ya wanajeshi wa Israel ya kuwauwa shahidi vijana 3 wa Nablus
Feb 10, 2022 23:00Katika hali ambayo wakazi wa Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan wameamua kufanya mgomo kama jibu lao kwa hatua ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuwauwa shahidi vijana watatu wa Kipalestina, maafisa wa utawala huo wametamka wazi kuwa Israel iko huru kufanya oparesheni yoyote ya mauaji.
-
Syria yazuia mashambulio ya Wazayuni dhidi yake
Feb 09, 2022 04:00Vyanzo vya Syria vimeripoti leo alfajiri kwamba mifumo ya ulinzi wa anga ya nchi hiyo imefanikiwa kuzuia mashambulio yaliyofanywa na utawala ghasibu wa Israel kuulenga mji mkuu wa nchi hiyo Damascus.
-
Kufutiwa utawala ghasibu wa Israel hadhi ya mwanachama mtazamaji katika Umoja wa Afrika
Feb 08, 2022 05:28Mkutano wa 35 wa wakuu wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika tarehe 5 na 6 za mwezi huu wa Februari huko Addis Ababa Ethiopia umesitisha hadhi ya utawala ghasibu wa Israel ya kuwa mwanachama mtazamaji katika umoja huo.
-
Syria yaipongeza AU kwa kusimamisha uanachama wa Israel katika jumuiya hiyo
Feb 07, 2022 23:19Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Syria imekaribisha uamuzi wa Umoja wa Afrika wa kusimamisha hadhi ya uanachama mwangalizi ya utawala wa Kizayuni Israel katika jumuiya hiyo.
-
Al Houthi: Uamuzi wa AU dhidi ya Israel ni pigo kubwa kwa wanaopatana na Wazayuni
Feb 07, 2022 03:52Mjumbe mmoja mwandamizi wa Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen amesema kuwa, hatua ya Umoja wa Afrika (AU) ya kuutimua utawala wa Kizayuni wa Israel kwenye umoja huo ni pigo kubwa kwa wale wanaojipendekeza kwa utawala huo dhalimu.