-
Mamlaka ya Ndani: Njia pekee ya kutatua mgogoro uliopo, ni kuundwa nchi huru ya Palestina
May 26, 2021 02:39Waziri wa Mambo ya Nje wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amesema kuwa, juhudi za kimataifa za kujaribu kuutatua kisiasa mgogoro wa Palestina hazitofanikiwa ila kwa kuundwa nchi huru ya Palestina mjini mkuu wake ukiwa ni Baytul Muqaddas.
-
HAMAS yawapa mbinu Wapalestina wa Quds za kupambana na Wazayuni
May 25, 2021 06:35Mjumbe mwandamizi wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amewataka Wapalestina wanaoishi katika mji mtakatifu wa Baytul Muqaddas kutotulia, bali waendelee kujibu jinai zote zinazofanywa na wanajeshi wa Israel na walowezi wa Kizayuni dhidi yao.
-
Ufaransa yakiri kuhusu utambulisho wa kigaidi wa utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina
May 25, 2021 06:03Jumapili iliyopita Jean-Yves Le Drian, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa aliashiria hujuma ya kinyama iliyofanywa karibuni na utawala haramu wa Israel katika miji kadhaa ya Waarabu katika ardhi unazozikalia kwa mabavu na kutahadharisha dhidi ya ubaguzi wa rangi unaotekelezwa na utawala huo dhidi ya Wapalestina.
-
Jordan yalaani uvamizi mpya wa utawala wa Kizayuni katika Msikiti wa al Aqsa
May 23, 2021 22:01Wizara ya Mambo ya Nje ya Jordan imelaani uvamizi mpya wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika Msikiti wa al Aqsa na hatua ya utawala huo ya kuwatia nguvuni wafanyazi wa Idara ya Waqfu ya Quds.
-
Wazayuni wazidi kupapurana, sasa mawaziri wawashambulia majenerali wa kijeshi kuhusu Ghaza
May 22, 2021 02:04Baraza la Mawaziri la utawala wa Kizayuni limelilaumu jeshi la utawala huo kwa kuboronga katika vita vilivyoisha juzi usiku vya Ukanda wa Ghaza.
-
Nchi 63 zalitaka Baraza la Haki za Binadamu la UN lichunguze jinai za Israel huko Palestina
May 21, 2021 21:59Nchi 63 zimelitaka Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa lifanye uchunguzi na kushughulikia jinai zilizofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya raia wasio na hatiai wa Palestina.
-
Ayatullah Makarim: Wazayuni wameionyesha dunia hulka yao ya ushenzi
May 20, 2021 23:07Ayatullah Nasir makarim Shirazi, mmoja wa Marjaa Taqlidi aliyeko mji mtukufu wa Qum amelaani hatua za kinyama zinazochukuliwa na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel za kuua na kumwaga damu za wanaume, wanawake na watoto madhulumu na wasio na ulinzi wa Palestina.
-
Silaha mpya za Marekani kwa utawala wa Israel; hatua nyingine ya kuendeleza mauaji dhidi ya Wapalestina
May 19, 2021 22:23Sambamba na kufikia kilele jinai za utawala wa kigaidi wa Israel dhidi ya Wapalestina, serikali ya Rais Joe Biden wa Marekani umeamua kuuzia utawala huo silaha mpya na za kisasa kabisa zenye thamani ya dola milioni 735.
-
Utawala wa Kizayuni wabomoa kikamilifu misikiti mitatu Gaza
May 19, 2021 06:53Utawala wa Kizayuni wa Israel mbali na kufanya mauaji dhidi ya Wapalestina katika hujuma na mashambulio yake ya kinyama yanayoendelea, umebomoa kikamilifu misikiti mitatu katika Ukanda wa Gaza.
-
Wazayuni: Hatujawahi kushambuliwa kwa idadi kubwa ya makombora kama mara hii
May 19, 2021 00:06Msemaji wa lugha ya Kiarabu wa jeshi la utawala katili wa Kizayuni usiku wa kuamkia leo amekiri kwamba utawala huo dhalimu haujawahi kushambuliwa kwa idadi kubwa ya makombora na makundi ya muqawama kama unavyoshambuliwa hivi sasa.