-
Waziri Mkuu wa Iraq: Jenerali Soleimani alikuwa bega kwa bega na Iraq katika nyakati ngumu kabisa
Jan 06, 2025 02:50Waziri Mkuu wa Iraq amemsifu na kumuenzi kamanda mkuu wa zamani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wa kupambana na ugaidi Luteni Jenerali Shahidi Qassem Soleimani, akisema, kamanda huyo alisimama bega kwa bega na nchi hiyo ya Kiarabu katika nyakati ngumu na za changamoto kubwa zaidi.
-
Kwa siku 3 Israel yashambulia zaidi ya mara 100 Ghaza, yaua Wapalestina zaidi ya 200, wengi wao ni wanawake na watoto
Jan 05, 2025 11:06Wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamewaua Wapalestina wasiopungua 88 katika muda wa siku moja katika maeneo kadhaa ya Ukanda wa Ghaza.
-
Utawala wa Kizayuni wakiri kuuliwa wanajeshi wake zaidi ya 800 na kujiuwa wengine 28
Jan 05, 2025 04:09Ikiwa imepita siku 456 tangu Israel ianzishe vita dhidi ya Gaza, utawala huo umekiri kuhusu baadhi ya maafa na vipigo ulivyopata tangu kutekelezwa Oparesheni ya Kimbunga cha al Aqsa na wanamuqawama wa Palestina.
-
Baraza la Usalama laitisha kikao kujadili hali ya Gaza
Jan 04, 2025 03:50Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeitisha kikao ambacho ajenda yake kuu ni kuchunguza mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
UN yatiwa wasiwasi na hali ya kiafya na kimatibabu ya Ukanda wa Gaza
Jan 03, 2025 08:34Wataalamu hao wa Umoja wa Mataifa wataka kukomeshwa upuuaji wa waziwazi' haki ya haki ya kiafya huko Gaza baada ya utawala wa Kizayuni wiki iliyopita kuishambulia Hospitali ya Kamal Adwan katika eneo hilo na kumtia nguvuni kihilela na kumuweka kizuizini Mkurugenzi wa hospitali hiyo Dakta Hussam Abu Safiya.
-
Watoto wachanga wapatao 1,100 wameuliwa katika vita vya Israel dhidi ya Ghaza
Jan 02, 2025 03:19Watoto wachanga Wapalestina wapatao 1,100 wameuawa katika mashambulio ya kinyama ya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel tangu Oktoba 2023.
-
Wanajeshi wa Israel waendelea kupokea vipigo kutoka kwa wanamapambano wa Palestina
Dec 30, 2024 23:21Kundi la Saraya al-Quds, Tawi la Kijeshi la Harakati ya Jihad al Islami ya Palestina, limetangaza kwamba limefanikiwa kutoa kipigo kipya na kikali mno kwa wanajeshi makatili na vamizi wa Israel huko Ghaza.
-
Wafanyakazi wa BBC wafichua mhariri wao alivyochangia 'kusafisha' jinai za kivita za Israel Ghaza
Dec 30, 2024 00:15Wafanyakazi wa Shirika la Utangazaji la Uingereza BBC wamefichua kuwa mhariri wao Raffi Berg ana udhibiti kamili wa ripoti zinazotolewa mitandaoni na shirika hilo kuhusu vita vya mauaji ya kimbari ya Israel huko Ghaza, na kuhakikisha kuwa habari zote zinazotolewa zinaipendelea Israel. Hayo ni kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotolewa na tovuti ya habari ya Drop Site News.
-
Mcheza chess wa Iran akataa kushindana na mpinzani wa Israel akiwaunga mkono Wapalestina
Dec 30, 2024 00:15Katika kuwaunga mkono watu wa Palestina, mchezaji wa chess wa Iran amekataa kushindana na mwakilishi wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika mashindano ya World Rapid Chess Championship 2024 huko New York.
-
Jinai za Israel zinaendelea: Wapalestina wengine 15 wauawa shahidi
Dec 27, 2024 07:38Wapalestina wengine 15 wameuawa shahidi katika jinai ya hivi punde ya jeshi la utawala wa Kizayuni katika ukanda wa Gaza.