-
Wahajiri kutoka Syria, kisingizio kinachotumiwa na Rais Erdoğan wa Uturuki kuushinikiza Umoja wa Ulaya
Mar 05, 2020 06:45Rais Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki amelikataa pendekezo la Umoja wa Ulaya kuhusu kadhia ya wahajiri na kusema: Hakuna mtu yeyote mwenye haki na ustahiki wa kuichezea ghururi ya Uturuki. Erdoğan ameyasema hayo mjini Ankara katika mkutano na waandishi wa habari aliofanya pamoja na Waziri Mkuu wa Bulgaria, Boyko Borisov.
-
Askari wa Uturuki wakimbia kwa makundi katika viunga vya Idlib, Syria + Video
Mar 04, 2020 13:24Kufuatia mashambulizi makali ya anga na mizinga ya jeshi la Syria dhidi ya maeneo ya jeshi la Uturuki katika viunga vya mkoa wa Idlib, askari wa Uturuki wameonekana wakikimbia kwa makundi katika maeneo hayo.
-
Malalamiko ya Ujerumani kwa hatua ya Uturuki ya kuzishinikiza nchi za Ulaya kupitia wakimbizi
Mar 04, 2020 08:12Kansela wa Ujerumani Angela Merkel ameitaja hatua ya Uturuki ya kutumia kadhia ya wakimbizi kuishinikiza Ulaya kuwa jambo lisilokubalika kufuatia nchi hiyo kufungua mipaka yake na kupelekea kumiminika Ulaya maelfu ya wakimbizi waliokuwa wakiishi katika kambi huko Uturuki.
-
Makumi ya maelfu ya wahajiri wavuka mpaka wa Uturuki na kuingia Ulaya
Mar 03, 2020 11:28Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki ametangaza kwamba hadi kufikia Jumapili usiku wahajiri wapatao laki moja walikuwa wamevuka mpaka wa nchi hiyo kuelekea Ugiriki na Bulgaria.
-
Putin: Moscow haina nia ya kuingia vitani na nchi yoyote
Mar 02, 2020 13:37Rais Vladimir Putin wa Russia ametoa radiamali yake kufuatia kushtadi mizozo kati ya nchi yake na Uturuki kuhusiana na kadhia ya Idlib, Syria na kusisitiza kwamba, Moscow haina nia ya kuingia vitani na nchi yoyote.
-
Kura ya turufu ya Ugiriki na hatua ya Uturuki ya kuwaweka rehani wakimbizi
Mar 01, 2020 10:39Uingiliaji wa wazi wa askari wa Uturuki katika mkoa wa Idlib nchini Syria, katika kuyaunga mkono makundi ya kigaidi yanayoendesha harakati zake mkoani humo, umepata uungaji mkono wa Wamagharibi.
-
Ugiriki yazuia kutolewa taarifa ya uungaji mkono wa NATO kwa Uturuki
Mar 01, 2020 02:39Serikali ya Ugiriki imetumia haki yake ya turufu kuzuia kutolewa taarifa ya uungaji mkono wa Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi (NATO) kwa Uturuki.
-
Wasiwasi wa Iran juu ya kushadidi machafuko katika eneo la magharibi mwa Asia
Feb 29, 2020 09:19Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetoa taarifa kuhusiana na yanayojiri katika eneo la Idlib nchini Syria na kueleleza wasiwasi wa Tehran kuhusu uwezekano wa kushadidi zaidi mivutano na machafuko katika eneo hilo. Taarifa hiyo pia imelaani hatua zinazofanywa na pande nyingine kwa ajili ya kukwamisha mwenendo wa mazungumzo ya Astana.
-
Kufeli siasa za Uturuki mkoani Idlib, Syria
Feb 29, 2020 02:38Wajumbe wa kisiasa wa Russia na Uturuki wamekutana mjini Ankara kujadiliana masuala ya kaskazini mwa Syria hasa ya mkoa wa Idlib.
-
Askari wengi wa jeshi la Uturuki waangamizwa kaskazini mwa Syria, Ankara yasema italipiza kisasi
Feb 28, 2020 07:54Vyombo vya habari katika eneo vimeripoti kuwa askari wasiopungua 33 wa jeshi la Uturuki wameangamizwa katika mkoa wa Idlib kaskazini magharibi mwa Syria.