-
Erdogan: Muuaji wa Khashoggi alisikika akisema 'Najua Namna ya Kukata'
Dec 15, 2018 11:07Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki amefichua kuwa katika sehemu ya faili la sauti kuhusu mauaji ya Jamal Khashoggi, mmoja kati ya wauaji wa mpinzani huyo wa utawala wa Saudia alisikika akijigamba kuwa, 'Najua namna ya kukata.'
-
Mkutano wa maspika wa mabunge ya nchi sita wamalizika mjini Tehran kwa kutoa taarifa
Dec 08, 2018 12:07Maspika wa mabunge ya nchi sita za Iran, Russia, Uturuki, China, Pakistan na Afghanistan umemalizika leo hapa mjini Tehran kwa taarifa ya pamoja ya kuimarisha uhusiano katika kupambana na ugaidi na kuongeza ushirikiano wao wa kieneo.
-
Mauaji ya Kashoggi; Uturuki yatoa waranti wa kukamatwa wapambe wa Bin Salman
Dec 05, 2018 23:14Mwendesha Mashitaka Mkuu wa mji wa Istanbul nchini Uturuki ametoa waranti wa kutiwa nguvuni wapambe wawili wa karibu wa Mohammad Bin Salman, Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudi Arabia, kwa tuhuma za kupanga mauaji ya Jamal Khashoggi, aliyekuwa mwandishi wa habari na mkosoaji wa utawala wa Aal-Saud.
-
Iran na Uturiki zahimizwa kukabiliana na ugaidi na propaganda chafu dhidi ya Uislamu
Dec 05, 2018 04:39Mkuu wa Jumuiya ya Masuala ya Dini nchini Uturuki amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Uturuki ambazo ni nchi kubwa zaidi katika eneo la Mashariki ya Kati zinapaswa kuzidisha ushirikiano kwa ajili ya kupambana na ugaidi na njama zinazoeneza propaganda za kuchafua sura safi ya Uislamu.
-
Iran na Uturuki zahimiza kufanikishwa biashara ya dola bilioni 30 baina yao
Nov 30, 2018 01:03Maspika wa mabunge ya Iran na Uturuki wamesisitizia haja ya kufanikishwa biashara ya dola bilioni 30 baina ya nchi zao.
-
Sisitizo la Umoja wa Ulaya na Uturuki la kuendelea kushirikiana na Iran
Nov 24, 2018 08:18Hatua ya rais wa Marekani, Donald Trump ya kuiondoa nchi hiyo katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na kuiwekea tena Iran vikwazo imepingwa vikali na nchi nyingine wanachama wa makubaliano hayo ya JCPOA yaani kundi la 4+1.
-
Uturuki: Maelezo ya Mwanasheria Mkuu wa Saudia kuhusu mauaji ya Khashoggi, hayatoshi
Nov 16, 2018 01:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Mevlüt Çavuşoğlu amekosoa maelezo ya Mwanasheria Mkuu wa Saudi Arabia kuhusiana na mauaji ya Jamal Khashoggi, mwandishi wa habari mkosoaji wa utawala wa Aal-Saud mjini Istanbul na kuongeza kwamba maelezo hayo hayatoshi kabisa.
-
"Saudia ilitumia programu ya udukuzi ya Israel kumfuatilia Kashoggi"
Nov 08, 2018 11:49Edward Snowden, afisa wa zamani wa Shirika la Usalama wa Taifa la Marekani (NSA) amefichua nafasi ya utawala haramu wa Israel katika mauaji ya kikatili ya mkosoaji wa utawala wa Saudi Arabia, Jamal Khashoggi yaliyofanywa na Riyadh nchini Uturuki mwezi uliopita.
-
Uturuki: Timu ya mauaji ya Khashoggi imefanya mauaji kama hayo huko nyuma
Nov 02, 2018 12:54Vyombo vya Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki vimefuichua kuwa, Ankara ina ushahidi unaothibitisha kuwa, timu ya mauaji ya Saudi Arabia iliyoshiriki katika mauaji ya kigaidi dhidi ya mwandishi na mkosoaji wa serikali ya kifalme ya nchi hiyo, Jamal Khashoggi mjini Istanbul yapata mwezi mmoja uliopita, iliwahi kufanya mauaji kadhaa kama hayo hapo kabla.
-
Erdogan aitaka Saudia imfichue aliyetoa agizo la kuua Jamal Khashoggi
Oct 26, 2018 11:37Kwa mara nyingine tena Rais Recep Tayyib Erdogan wa Uturuki ameitaka Saudi Arabia imfichue mtu ambaye alitoa amri ya kuuawa Jamal Khashoggi, mwandishi wa habari na mkosoaji mkubwa wa utawala wa Aal-Saud.