-
Maduro afichua mpango wa Marekani na Colombia wa kutaka kumuuwa
Sep 23, 2019 02:47Rais wa Venezuela amefichua mpango wa kutaka kumuuwa unaofanywa kwa siri na rais wa zamani wa Colombia kwa kushirikiana na Marekani.
-
Venezuela: Tutaichukulia hatua Colombia katika Umoja wa Mataifa
Sep 02, 2019 04:06Serikali ya Venezuela imesema kuwa itawasilisha ushahidi kwa Umoja wa Mataifa kuhusu misaada na uungaji mkono unaotolewa na Colombia kwa makundi yanayobeba silaha ya upinzani dhidi ya serikali ya Rais Maduro.
-
Mazungumzo ya Marekani na serikali ya Venezuela; kulegeza kamba Trump kuhusu mpango wake wa kuipindua serikali ya Maduro
Aug 22, 2019 06:28Baada ya miezi kadhaa ya njama za Marekani za kutaka kuipindua serikali ya Rais Nicolas Maduro wa Venenzuela, hivi sasa Washington imekata tamaa na siasa zake za kibabe na imebadilisha msimamo wake kikamilifu kwa kufanya mazungumzo na viongozi kadhaa wa Caracas.
-
Maduro akosoa hatua za Trump dhidi ya Venezuela
Aug 20, 2019 02:33Kufuatia kuendelea vitisho na mashinikizo ya Marekani dhidi ya Venezuela, Rais Nicolas Maduro wa nchi hiyo amekosoa hatua za Rais Donald Trump dhidi ya nchi yake na kusema: "Hatua ambazo Rais wa Marekani anachukua dhidi ya Venezuela ni sawa na zile ambazo kiongozi wa Wanazi alichukua katika Vita Vikuu vya Pili vya Dunia."
-
Maduro afichua: Marekani na Colombia zimepanga njama ya kuniua
Aug 15, 2019 09:35Rais Nicolás Maduro wa Venezuela amefichua kwamba, rais wa zamani wa Colombia ameajiri makumi ya mamluki waliopewa jukumu la kumuua yeye.
-
Serikali ya Venezuela yasimamisha mazungumzo na wapinzani kulalamikia vikwazo vya Marekani
Aug 10, 2019 01:17Marekani ikiwa ni nchi inayoingilia wazi wazi masuala ya ndani ya Venezuela imefanya juhudi nyingi za kuipigisha magoti serikali ya mrengo wa kushoto ya nchi hiyo na pia kujaribu kumng'oa madarakani Rais Nicolas Maduro wa nchi hiyo lakini bila mafanikio yoyote.
-
John Bolton aingilia tena masuala ya ndani ya Venezuela
Aug 07, 2019 01:19Mshauri wa Usalama wa Taifa wa Marekani amesema kuwa Washington inapinga kufanyika uchaguzi mpya nchini Venezuela madhali Rais wa sasa wa nchi hiyo ataendelea kusalia madarakani.
-
Tuhuma za Marekani dhidi ya Russia kwa kuisaidia Venezuela
Jul 23, 2019 07:33Katika kipindi cha utawala wa Rais Donald Trump wa Marekani, siasa za upande mmoja za Washington dhidi ya nchi tofauti zinazopinga ubeberu na kupenda makubwa kwa Marekani, ikiwemo Venezuela , zimebadilika kuwa moja ya tofauti za msingi kati ya serikali ya Moscow na Washington.
-
Jumuiya ya NAM yasisitiza kuheshimiwa mitazamo ya pande kadhaa na sheria za kimataifa
Jul 22, 2019 05:55Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote NAM, wamekutana huko Caracas, mji mkuu wa Venezuela na kusisitiza umuhimu wa kuzingatiwa mitazamo ya pande kadhaa na kueshimiwa sheria za kimataifa.
-
Kuendelea mazungumzo ya serikali ya Venezuela na wapinzani licha ya vitisho vya Wamagharibi
Jul 21, 2019 07:49Mashinikizo na vitisho vya Marekani na nchi za Ulaya dhidi ya Venezuela, vimeongezeka huku mazungumzo ya kutafuta njia ya kuiodoa nchi hiyo kwenye mgogoro wa kisiasa yakiwa yanaendelea kati ya serikali na wapinzani.