Ripoti ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa imetoa pendekezo kwa askari wa kulinda amani wa umoja huo kutumia 'nguvu' kuzima tishio dhidi yao wanapolazimika kufanya hivyo wakiwa katika operesheni zao.
Wanajeshi watatu wa Kikosi cha Kusimamia Amani cha Umoja wa Mataifa nchini Mali MINUSMA wameuawa katika mripuko wa bomu uliotokea kaskazini mwa nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika.
Watu karibu 30 wameuawa na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa katika mapigano mapya yaliyozuka kati ya vikosi vya majimbo mawili hasimu yenye mamlaka ya ndani nchini Somalia.
Uganda imetangaza kuwa itaondoa askari wake walioko nchini Somalia chini ya mwavuli wa Kikosi cha Kusimamia Amani cha Umoja wa Afrika AMISOM kufikia mwishoni mwa mwaka ujao 2017.