-
Ujumbe mbalimbali wa operesheni ya kulipiza kisasi ya jeshi la Yemen dhidi ya Saudia
Jun 25, 2020 09:39Brigedia Jenerali Yahya Saree, Msemaji wa Majeshi ya Yemen, Jumanne tarehe 23 Juni alitangaza habari ya kufanyika operesheni kubwa ya kijeshi ya kulipiza kisasi cha jinai zinazofanywa na Saudi Arabia dhidi ya wananchi wa Yemen.
-
Vita vya maneno vyashtadi kati ya Imarati na Uturuki
May 02, 2020 01:36Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki imeitaka Imarati kukomesha misimamo yake ya uhasama dhidi ya nchi hiyo.
-
Kushadidi vita nchini Libya katika kivuli cha virusi vya Corona
Apr 14, 2020 11:13Licha ya kuibuka virusi vya Corona na kuenea kote ulimwenguni na hilo kupelekea kusitishwa vita na mapigano katika maeneo mengi ya dunia, lakini nchini Libya kwa sasa vita vimeshika kasi.
-
Wasi wasi wa Umoja wa Ulaya kuhusu kuendelea mapigano nchini Yemen, undumakuwili wa EU
Apr 01, 2020 09:41Tangu mwezi Machi 2015, Saudi Arabia iliunda muungano kwa kushirikiana na Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) na kuanzisha vita vya kidhalimu dhidi ya watu wa Yemen na hadi sasa makumi ya maelfu ya raia wa nchi hiyo wameshauawa shahidi na kujeruhiwa.
-
Tripoli yaitaka Khartoum kuwaondoa mamluki wa Kisudani nchini Libya
Mar 21, 2020 11:47Mjumbe katika Baraza la Utawala la Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa nchini Libya, Muhammad Ammari amesema Libya ingali inasubiri ufafanuzi wa Serikali ya Sudan kuhusu uwepo wa mamluki wa Kisudani katika safu za wapiganaji wa jenerali muasi, Khalifa Haftar wanaoendelea kuhujumu mji wa Tripoli.
-
Makamanda wa jeshi la Ethiopia wasema wako tayari kukabiliana na hujuma yoyote ya Misri
Mar 14, 2020 12:38Mkuu wa majeshi ya Ethiopia amesema kuwa jeshi la nchi hiyo liko tayari kukabiliana na hujuma ya aina yoyote ya kijeshi itakayolenga bwawa la al Nahdha na kujibu hujuma hiyo.
-
Indhari ya UN kuhusu kubadilika mzozo wa Libya kuwa vita vya kieneo
Mar 02, 2020 00:20Licha ya mazungumzo na juhudi za kimataifa katika wiki za hivi karibuni kwa ajili ya kuhitimisha vita nchini Libya, lakini mapigano yamezidi kuongezeka na sasa nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika imegeuka kuwa ulingo wa vita vya niaba.
-
Saudia imeshindwa katika vita dhidi ya Yemen
Feb 16, 2020 11:00Kuvunjika makubaliano ya Riyadh, kuondoka kikamilifu askari wa Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) kutoka Yemen na kutunguliwa ndege ya kivita aina ya Tornado ya muungano vamizi wa Saudia, kabla ya jambo lolote lile, ni mambo yanayoashiria kushindwa serikali ya Riyadh katika vita vyake vya kichokozi dhidi ya Yemen.
-
Vijana wa Sudan wasimulia jinsi Abu Dhabi ilivyowapeleka kupigana vita Libya
Feb 16, 2020 02:51Vijana wa Kisudan waliorejea makwao hivi karibuni wamesimulia jinsi walivyohadaiwa na kampuni ya Black Shield Security Services iliyowaahaidi kuwapa kazi za ulinzi na badala yake walijikuta wakipewa mafunzo ya kijeshi yasiyooana na kazi zao na kupelekwa bila ya kujua huko Libya na Yemen kupigana vita.
-
Ripoti ya Independent: Kengele za vita zasikika zaidi katika milango ya Libya
Jan 29, 2020 15:05Ripoti iliyotolewa na gazeti la Independent la Uingereza imefichua kuwa, mapatano tete ya kusitisha vita yaliyofikiwa hivi karibuni baina ya madola makubwa mjini Berlin huko Ujerumani yanaelekea kuporomoka kutokana na mashambulizi ya anga yanayoshuhudiwa sasa nchini Libya na vitisho vinavyoendelea kutolewa na pande hasimu.