-
Mbunge wa Kongresi: Ni mwehu anayedai Marekani imeshinda vita dhidi ya Iran
May 02, 2026 07:25Mwakilishi wa cha cha Democratic wa California katika Kongresi ya Marekani, Sara Jacobs, amemkosoa vikali Waziri wa Vita wa nchi hiyo, Pete Hegseth kwa kutangaza ushindi dhidi ya Iran, akitaja madai hayo kuwa ni udanganyifu.
-
Jeshi la Mali lakomboa mji wa mpakani baada ya shambulio la ISIS karibu na Niger
May 02, 2026 07:21Vikosi vya jeshi la Mali vimedhibiti tena mji wa karibu na mpaka wa nchi hiyo na Niger baada ya wanamgambo wanaohusishwa na ISIS kuondoka katika eneo hilo kufuatia mapigano makali, wakati jeshi likiimarisha doria kwenye maeneo hayo.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan: Tumekataa majaribio ya kulazimisha masuluhisho kutoka nje
May 02, 2026 06:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan, Mohi El-Din Salem, amefichua kwamba serikali ya nchi yake itafanya tathmini ya uhusiano wake wa kimataifa na kikanda baada ya vita, na hautakuwa sawa na hapo awali. Amesema kuwa wizara yake imezuia majaribio ya kulazimisha masuluhisho ya kigeni kwa nchi yake na haitakubali mashinikizo ya aina yoyote.
-
Mkuu wa Jeshi la Wanamaji la Iran: Wamarekani wanaogopa silaha yetu mpya
Apr 30, 2026 10:57Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amesema kwamba majeshi ya Iran yameufunga Mlango Bahari wa Hormuz kutoka Bahari ya Arabia, akisisitiza kwamba: Adui atakutana na silaha yetu ambayo anaiogopa sana.
-
Kukiri Washirika wa Marekani Kwamba Nchi Hiyo Imeshindwa Katika Vita Dhidi ya Iran
Apr 30, 2026 04:31Baada ya kupita takribani miezi miwili tangu Marekani na utawala wa kizayuni zilipoanzisha uvamizi wa kijeshi dhidi ya Iran, wakosoaji wa sera za kushupalia vita za Trump katika kila pembe ya dunia wanaendelea kukiri na kutamka kwa uwazi zaidi kwamba Marekani imeshindwa katika vita hivyo.
-
Ripoti: Viongozi wa RSF wamejenga na kulimbikiza mali za mamilioni ya pesa kwa himaya ya Imarati
Apr 28, 2026 09:34Viongozi wa wanamgambo wa Sudan wanaojulikana kwa jina la Kikosi cha Msaada wa Haraka au Rapid Support Forces (RSF) na mtandao wao wamekusanya mamilioni ya mali za kifahari huko Dubai katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).
-
Rais Pezeshkian: Iran haitaingia katika mazungumzo chini ya mashinikizo, vitisho na mzingiro
Apr 26, 2026 09:34Rais Masoud Pezeshkian amekosoa utata na mgongano unaoshuhudiwa kati ya mbinu za mashinikizo zinazotumiwa na Marekani dhidi ya Iran na kile kinachotajwa kuwa ni nia yake ya kushiriki katika mchakato wa kidiplomasia na Jamhuri ya Kiislamu.
-
Aljazeera: Trump anatafuta njia ya kutoka vitani kwa heshima
Apr 19, 2026 10:51Mwandishi wa kituo cha Aljazeera huko Washington anasema kuwa Rais Donald Trump Marekani anatafuta jinsi ya kutoka kwenye vita na Iran kwa njia ya heshima.
-
Wall Street Journal: Kambi ya Diego Garcia imeshambuliwa kwa makombora ya Iran
Mar 21, 2026 06:36Gazeti la Kimarekani la Wall Street Journal limeripoti kwamba, Iran imeshambulia kwa makombora mojawapo ya kambi za mbali zaidi za kistratijia za jeshi la Marekani nje ya nchi hiyo.
-
Indhari ya Gavana wa Benki Kuu ya US kuhusu taathira za kupanda gharama za maisha kutokana na vita na Iran
Mar 19, 2026 07:23Gavana wa Benki Kuu ya Marekani ametahadharisha kuhusu athari mbaya za vita dhidi ya Iran kwa uchumi wa Marekani na kuongezeka gharama za maisha nchini humo.