Jul 11, 2023 11:30
Mapigano nchini Sudan yanaendelea kupamba moto, na juhudi zilizofanywa hadi sasa za kuleta suluhu na kurejesha amani na utulivu katika nchi hiyo sio tu hazijafanikiwa, lakini pande mbili zinazopigana zimeshadidisha pia mashambulizi yao. Kutokana na hali hiyo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametahadharisha kuwa, Sudan sasa imeshafika kwenye ukingo wa vita kamili vya wenyewe kwa wenyewe.