-
Jarida la Wall Street: Imarati imetuma silaha kwa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) huko Sudan
Aug 11, 2023 07:56Jarida la Kimarekani la Wall Street Journal limefichua katika ripoti yake kwamba Umoja wa Falme za Kiarabu unatoa misaada ya kijeshi kwa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), vinavyopigana na jeshi la Sudan kwa miezi kadhaa sasa.
-
Amnesty International: Uhalifu wa kutisha wa kivita unafanyika nchini Sudan
Aug 04, 2023 12:09Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limesema katika ripoti yake mpya kwamba uhalifu mkubwa wa kivita unafanywa nchini Sudan, na kwamba raia kote nchini humo wanaishi katika hufo na woga "usiofikirika".
-
Indhari ya Katibu Mkuu wa UN ya kufikia Sudan kwenye ukingo wa vita kamili vya wenyewe kwa wenyewe
Jul 11, 2023 11:30Mapigano nchini Sudan yanaendelea kupamba moto, na juhudi zilizofanywa hadi sasa za kuleta suluhu na kurejesha amani na utulivu katika nchi hiyo sio tu hazijafanikiwa, lakini pande mbili zinazopigana zimeshadidisha pia mashambulizi yao. Kutokana na hali hiyo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametahadharisha kuwa, Sudan sasa imeshafika kwenye ukingo wa vita kamili vya wenyewe kwa wenyewe.
-
Wafadhili waahidi kutoa msaada wa dola bilioni 1.5 kwa ajili ya Sudan
Jun 20, 2023 08:05Wafadhili wameahidi katika Mkutano wa Geneva wa Kukabiliana na Mgogoro wa Sudan, kutoa msaada wa kibinadamu wa takriban dola bilioni 1.5, wakati huu ambapo hali ya utulivu imetanda kwa kiasi fulani nchini Sudan kwa siku ya pili kutokana na makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyofikiwa baina ya jeshi la Sudan na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF).
-
UN yalaani ukiukwaji wa makubaliano ya kusitisha vita Sudan, mapigano makali yaripotiwa Khartoum
May 19, 2023 10:31Mjumbe wa Umoja wa Mataifa anayehusika na masuala ya kibinadamu, Martin Griffiths, amelaani kile alichokitaja kuwa ukiukwaji wa mara kwa mara na mkubwa wa makubaliano yaliyofikiwa wiki moja baina ya pande zihasimu katika mzozo wa Sudan ya kulinda maisha ya raia, harakati za misaada ya kibinadamu na miundombinu.
-
Mapigano ya kuwania madaraka baina ya majenerali yaingia siku ya pili nchini Sudan
Apr 16, 2023 10:26Mapigano kati ya jeshi la Sudan na Vikosi vya Radiamali ya Haraka yameingia siku ya pili, huku milipuko ikisikika tangu alfajiri ya leo, Jumapili, karibu na Mji wa Michezo, kusini mwa mji mkuu, Khartoum.
-
Kuwa wakimbizi mamilioni ya watu duniani ni matokeo ya vita vya Marekani baada ya Septemba 11
Apr 10, 2023 11:46Vita vilivyoanzishwa na Marekani baada ya mashambulizi ya Septemba 11 mwaka 2001 nchini humo yamepelekea zaidi ya watu milioni 37 duniani kuwa wakimbizi.
-
Seneti ya Marekani yafuta kibali cha Pentagon kuhusu oparesheni za kijeshi Iraq
Apr 01, 2023 03:13Seneti ya Marekani Jumatano wiki hii ilihitimisha kibali ilichokuwa imekitoa kwa Wizara ya Ulinzi ya nchi hiyo (Pentagon) mwaka 1999 na 2002 kwa ajili ya vita huko Iraq na imepasisha uamuzi wa kufutwa kibali cha Pentagon kwa ajili ya kutekeleza oparesheni za kijeshi huko Iraq bila ya kuhitaji idhini ya Kongresi.
-
Maandamano dhidi ya vita katika nchi za Ulaya
Feb 27, 2023 11:44Sambamba na kuendelea vita nchini Ukraine na hali mbaya ya kiuchumi na kijamii katika nchi mbalimbali za Ulaya, wananchi barani humo wamefanya maandamano katika nchi kadhaa wakipinga sera za nchi za Magharibi na kuingilia kati vita vya Ukraine.
-
Mwito wa Russia wa kufuatiliwa jinai za Marekani na Uingereza nchini Iraq
Feb 10, 2023 04:06Vasily Nebenzya, mwakilishi wa kudumu wa Russia katika Umoja wa Mataifa, Jumatano ya juzi na ikiwa ni siku tatu baada ya kumbukumbu ya mwaka wa uongo mkubwa wa Marekani dhidi ya Iraq alisema kuwa, lazima watenda jinai Wamarekani na Waingereza wapandishwe kizimbani kwa jinai zao nchini humo.