-
Macron aendeleza vitendo vya kuuhujumu Uislamu; Trump aparamia mawimbi
Oct 31, 2020 02:38Kushtadi vitendo vya chuki na hujuma dhidi ya Uislamu nchini Ufaransa vinavyokwenda sambamba na uungaji mkono wa Rais wa nchi hiyo Emmanuel Macron kwa kisingizio kutetea uhuru wa kusema na kujieleza kumekabiliwa na radiamali mbalimbali na kuifanya nchi hiyo kubwa ya Ulaya ikabiiwe na wimbi kubwa la hasira.
-
Radiamali ya kindumakuwili ya Ufaransa kufuatia malalamiko ya Waislamu duniani
Oct 28, 2020 07:41Waislamu duniani kote wamekasirishwa na kushadidi vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu nchini Ufaransa hasa cha kuchapishwa tena katuni zinazomvunjia heshima Mtume Muhammad SAW. Hasira za Waislamu zimeongezeka maradufu baada ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa kutetea vitendo hivyo vya chuki dhidi ya Uislamu kwa kisingizo cha uhuru wa maoni.
-
Waislamu wasisitiza kususiwa bidhaa za Ufaransa, Macron asema Paris haitasitisha matusi dhidi ya Mtume (saw)
Oct 26, 2020 03:22Malalamiko na ukosoaji dhidi ya matamshi yaliyotolewa na Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa akitetea vitendo vya kutusiwa na kuvunjiwa heshima Mtume Muhammad (saw) nchini humo unaendelea kupamba moto huku nchi mbalimbali za Kiislamu zikitoa wito wa kuiadhibu Paris kwa kususia bidhaa za Ufaransa.
-
Waislamu wafukuzwa Ufaransa kwa kisingizio cha kupambana na misimamo mikali
Oct 20, 2020 02:29Mwenendo wa kuenezwa chuki na kejeli dhidi ya itikadi za Kiislamu umekuwa ukiongezeka kwa kasi kubwa nchini Ufaransa katika miaka ya karibuni.
-
Jitihada za Macron za kuhalalisha muswada dhidi ya Uislamu nchini Ufaransa
Oct 04, 2020 02:43Hujuma na vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu barani Ulaya viliongezeka sana baada ya matukio ya Septemba 11 mwaka 2001 nchini Marekani; na mashambulizi ya kundi la kigaidi na lenye misimamo mikali la Daesh katika baadhi ya nchi za Ulaya kama Ufaransa na Uingereza yamezidisha chuki na uhasama dhidi ya Waislamu. Hivi sasa serikali ya Ufaransa ina mpango wa kupasisha sheria ya kuimarisha hujuma na vita dhidi ya Uislamu.
-
Hatua za mwanasiasa mwenye chuki dhidi ya Uislamu nchini Uholanzi
Dec 30, 2019 02:41Geert Wilders, Mwanasiasa mwenye chuki dhidi ya Uislamu nchini Uholanzi sambamba na kutoa mwaliko, ametaka kufanyika mashindano ya vibonzo vya kumdhalilisha Mtume Muhammad (saw) kwa lengo la kujeruhi hisia za Waislamu.
-
Watu wenye chuki watishia kulipua kwa bomu msikiti mjini Berlin, Ujerumani
Nov 26, 2019 04:39Viongozi wa msikiti wa Sehitlik mjini Berlin, mji mkuu wa Ujerumani wametangaza kwamba watu wenye chuki dhidi ya dini ya Uislamu miongoni mwa makundi ya mrengo wa kulia na yenye misimamo ya kigaidi, wametishia kulipua kwa bomu msikiti huo.
-
Waislamu wa Norway kuwashitaki walioivunjia heshima Qur'an Tukufu
Nov 20, 2019 02:31Viongozi wa Kiislamu nchini Norway wametangaza kwamba wamekusudia kuwasilisha mashtaka kwa jeshi la polisi la nchi hiyo kufuatia kitendo cha kuichoma moto Qur'an Tukufu kilichojiri katika mkusanyiko mmoja wa maandamano hivi karibuni.
-
Waislamu wa Ufaransa ni wahanga wa ubaguzi wa kidini
Nov 07, 2019 12:43Karibu nusu ya Waislamu wanaoishi nchini Ufaransa, ni wahanga wa vitendo vya ubaguzi.
-
Rais wa Ufaransa atuhumiwa kueneza chuki dhidi ya Waislamu
Nov 05, 2019 02:31Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa ametuhumiwa kuhusika na kueneza chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu katika nchi hiyo ya Ulaya.