-
Askari usalama Nigeria wawakamata wanachama 40 wa genge lenye silaha
Apr 27, 2021 07:16Kikosi cha usalama nchini Nigeria ckimewatia nguvuni wanachama 40 wa genge la watu waliokuwa na silaha wakati wa operesheni iliyofanyika katika jimbo la kusini la Edo.
-
Waasi 21 wa kundi la CODECO wauawa DRC
Oct 27, 2020 11:17Waasi 21 wameuawa katika kipindi cha siku tatu za mapigano baina yao na jeshi la serikali katika mkoa wa Ituri, kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
-
Watoto wasiopungua 6 wauawa katika shambulio la waasi nchini Cameroon
Oct 25, 2020 08:20Watoto wasiopungua 6 wameuawa katika shambulio la watu wenye silaha lililolenga shule ya Fransisca International Bi-lingual Academy. Shambulio hilo lilifanyika jana katika eneo la Koumba kusini magharibi mwa Cameroon.
-
Sudan na kundi kuu la waasi zakubaliana kuanzisha tena mazungumzo ya amani
Sep 05, 2020 02:33Serikali ya Sudan na kundi kuu la waasi linaloendesha harakati zake katika maeneo ya mpakani ya kusini mwa nchi hiyo zimeafikiana kuanzisha tena mazungumzo amani chini ya uwenyeji wa Sudan Kusini.
-
Watu 13 wauawa katika shambulio la genge la waasi wa ADF mashariki mwa Congo
Aug 22, 2020 12:19Watu wasiopungua 13 wameuawa katika shambulio lililofanywa na waasi wa kundi la The Allied Democratic Forces (ADF) kutoka Uganda huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
-
Waasi waua wanajeshi watano na raia wanne nchini Cameroon
Mar 09, 2020 04:34Waasi wamemeshambulia kituo cha polisi kilichoko wilayani Galim magharibi mwa Cameroon na kuua wanajeshi watano na raia wanne.
-
Jeshi la Somalia lapambana na wanamgambo wa Ahlu Sunnah Wal Jama’a (ASWJ)
Feb 28, 2020 13:09Jeshi la Somalia mapema leo Ijumaa limepambana na wanamgambo wa kundi moja la kikanda katika kile kinachotajwa na Wasomali kuwa ni mapigano makali zaidi baada ya misuguano ya kisiasa inayoendelea kuikwamisha nchi hiyo katika dimbwi la ghasia na machafuko.
-
Jeshi la Sudan lazima uasi wa maafisa wa zamani wa utawala wa Al-Bashir
Jan 15, 2020 08:04Mkuu wa Baraza la Utawala la Sudan Luteni Jenerali Abdel Fattah al-Burhan amesema, anga ya nchi hiyo imefunguliwa tena na majengo yote ya Shirika la Intelijensia hivi sasa yanadhibitiwa na jeshi, kufuatia uasi uliofanywa na maafisa wa zamani wa usalama wa utawala wa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Omar al-Bashir.
-
Jeshi la Congo lamuua kiongozi wa tawi la waasi wa FDLR kutoka Rwanda
Nov 11, 2019 03:40Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo limetangaza kuwa limemuua kiongozi wa tawi lililojitenga la kundi la waasi wa Kihutu la Democratic Forces for the Liberation of Rwanda (FDLR) mashariki mwa nchi hiyo.
-
Kiongozi wa wasi wa FDLR kutoka Rwanda auawa huko Congo DR
Sep 19, 2019 07:40Kiongozi wa waasi wa Kihutu kutoka Rwanda aliyekuwa akisakwa na Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kwa tuhuma za kufanya jinai za kivita ameuawa kwa kipigwa risasi na askari wa jeshi la Congo.