Jul 15, 2019 10:24
Muungano wa Uhuru na Mabadiliko nchini Sudan umetangaza kuwa, mkutano uliokuwa umepangwa kufanyika leo na wawakilishi wa Baraza la Kijeshi linalotawala nchi hiyo chini ya upatanishi wa Ethiopia na Umoja wa Afrika umeakhirishwa hadi Jumanne ya kesho.