Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa limesema raia 232 wameuawa katika mashambulizi yaliyofanywa katika maeneo ya Mayendit na Leer nchini Sudan Kusini.
Pande hasimu Sudan Kusini zimeafiki kugawana madaraka kwa mujibu wa makubaliano yaliyofikiwa na pande hizo ambapo kwa mujibu wake kiongozi wa waasi nchini humo, Riek Machar atarejeshwa katika wadhifa wa Makamu wa Rais.
Kundi la waasi la Patriotic Ginbot7 (PG7) la Ethiopia limetangaza uamuzi wa upande mmoja wa kusimamisha kwa muda usiojulikana operesheni zake zote za utumiaji silaha katika maeneo yote ya nchi.
Waasi wa Sudan Kusini wametangaza kuwa muda zaidi unahitajika ili kufanikisha mchakato wa amani ya kudumu nchini humo na kwamba itakuwa jambo la muhimu kuvipatia ufumbuzi vyanzo vikuu vya vita vya wenyewe kwa wenyewe huko Sudan Kusini.
Viongozi wawili wa kundi la waasi wa Ethiopia wamerudi nyumbani baada ya kufanya mazungumzo na waziri mkuu wa nchi hiyo Abiy Ahmed Ali..
Shirika la kimataifa la kutetea haki za watoto walioathiriwa na migogoro duniani la War Child limesema aghalabu ya watoto wadogo wanaoujiunga na makundi ya waasi wanaobeba silaha katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wanafanya hivyo kwa khiari kwa sababu hawana chaguo mbadala.
Utendaji dhaifu wa jeshi la serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika kukabiliana na waasi wa maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo, umewakasirisha wakazi wa maeneo hayo na kuamua kufanya maandamano.
Askari watano na dereva mmoja wameuawa katika Mbuga ya Wanyamapori ya Virunga huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Waasi wenye silaha wamewauwa raia wasiopungua 11 katika shambulio moja kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Raia wengine wasiopungua elfu moja wameshauliwa na waasi hao hadi hivi sasa tangu mwaka 2014 katika mashambulizi kama hayo.
Waasi wa Uganda wa ADF-Nalu wamefanya tena mashambulio katika eneo moja mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kuua watu saba.