-
Waislamu Uingereza wawasaidia wenye mahitaji wakati huu wa mripuko wa Corona
Mar 19, 2020 03:58Waislamu nchini Uingereza, mijini na vijijini wanafanya jitihada za kukusanya bidhaa muhimu za msingi kwa ajili ya kuwasaidia watu wenye mahitaji na wasiojiweza nchini humo, katika kipindi hiki cha mripuko wa Corona.
-
Mwaka mmoja baada ya mauaji ya Waislamu New Zealand, usiri unatawala uchunguzi kuhusu mauaji hayo
Mar 14, 2020 22:58Ripoti iliyotayarishwa na gazeti la Washington Post inasema kuwa, uchunguzi wa serikali ya New Zealand wa kutaka kupata majibu yanayoweka wazi jinsi mhalifu aliyefanya mauaji ya kutisha ya Waislamu 51 waliokuwa wakitekeleza ibada misikitini, alivyoweza kufanya mauaji hayo, unaendelea kwa usiri mkubwa, jambo ambalo limezusha wasiwasi wa wachambuzi wa mambo ya jamii ya Waislamu wa New Zealand.
-
Ayatullah Hamedani alaani ukatili unaofanywa nchini India dhidi ya Waislamu
Mar 06, 2020 09:07Ayatullah Nouri Hussein Hamedani ambaye ni miongoni mwa viongozi wa juu wa kidini nchini Iran amelaani ukatili na mauaji yanayoendelea kufanywa dhidi ya Waislamu nchini India na kukosoa kimya cha vyombo vya habari duniani kuhusiana na mauaji hayo.
-
Kiongozi Muadhamu: India isitishe mauaji ya Waislamu iwapo haitaki kutengwa
Mar 05, 2020 09:55Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameitahadharisha serikali ya India dhidi ya kuendelea kutekeleza mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu wa nchi hiyo na kusisitiza kuwa, ukandamizaji unaoendelea kufanyiwa Waislamu katika nchi hiyo ya kusini mwa Asia utapelekea serikali ya New Delhi itengwe katika ulimwengu wa Kiislamu.
-
Zarif akosoa ukatili na ghasia zilizopangwa dhidi ya Waislamu India
Mar 03, 2020 04:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu inalaani vikali ukatili na ghasia zilizoratibiwa dhidi ya Waislamu nchini India, akisisitiza kuwa njia pekee ya kutatua mgogoro uliopo ni kufuata sheria na mazungumzo ya amani.
-
Ethiopia yatambua rasmi Baraza Kuu la Waislamu baada ya juhudi za miaka 60
Jan 26, 2020 03:40Baada ya juhudi za miaka 60 hatimaye Baraza Kuu la Waislamu nchini Ethiopia limetambuliwa rasmi na serikali ya Addis Ababa, suala ambalo limetajwa na wachambuzi wa mambo kuwa ni mafanikio ya kihistoria kwa wafuasi wa dini hiyo nchini Ethiopia.
-
Middle East Eye: Saudia inazidisha mashaka ya Waislamu wa Rohingya
Jan 07, 2020 23:18Kituo cha habari cha Middle East Eye kimeripoti kuwa, Saudi Arabia inazidisha mashaka na masaibu ya Waislamu wa jamii ya Rohingya huko Myanmar kwa kuwasaka, kuwakamata na kuwafukuza Warohingya wanaofanya kazi nchini humo.
-
Umoja wa Mataifa wailaani Myanmar kwa kuwandamiza Waislamu Warohingya
Dec 28, 2019 23:23Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepasisha azimio ambalo linailaani vikali Myanmar kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya na jamii za wengine waliowachache katika nchi hiyo ya Mabuddha.
-
Mahathir Mohammad.: Malaysia itawapa hifadhi wakimbizi wa Uyghur kutoka China
Dec 27, 2019 09:14Waziri Mkuu wa Malaysia Mahathir Mohammad amesema kuwa nchi yake haitawarejesha makwao Waislamu wa jamii ya Uyghur kutoka China iwapo wataomba hifadhi nchini humo.
-
Maandamano yashtadi nchini India kufuatia kupitishwa muswada ulio dhidi ya Waislamu
Dec 14, 2019 21:42Maandamano ya kupinga muswada wa uraia nchini India na ambao uko dhidi ya Waislamu, yameendelea kupanua wigo wake ambapo baada ya majimbo ya kaskazini mashariki, pia yamesambaa katika maeneo mengine kama vile Uttar Pradesh, Bihar na New Delhi.