-
Jumuiya ya Kiislamu yasisitizia umoja na kuwa macho Waislamu
Nov 17, 2019 07:35Viongozi wa Kiislamu kutoka nchi mbalimbali duniani walioshiriki mkutano wa 12 wa Baraza Kuu la Jumuiya ya Kimataifa ya Mwamko wa Kiislamu hapa Tehran wamesisitizia udharura wa kudumishwa umoja na mshikamano miongoni mwa Waislamu kote duniani.
-
Waislamu Uingereza waanzisha oparesheni ya kumtimua Boris Johnson
Nov 13, 2019 13:32Kundi moja la Waislamu Uingereza limeanzisha kampeni mpya inayojulikana kama "Oparesheni ya Kura ya Waislamu' kuwatimua wabunge wasio zingatia maslahi yao.
-
Waislamu Ujerumani wazidi kuandamwa na vitendo vya chuki na ubaguzi
Nov 03, 2019 02:32Mmoja wa viongozi wa Kiislamu nchini Ujerumani amesema kuwa, Waislamu wa nchi hiyo ya bara Ulaya wanazidi kuandamwa na mashambulio ambayo chimbuko lake ni vitendo vya ubaguzi na chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu.
-
Shule za Kiislamu Uingereza zaweka historia, zashika nafasi tatu za juu na kuongoza kwa ubora
Nov 02, 2019 08:14Shule za Kiislamu za Uingereza zimeweka historia kwa kushika nafasi tatu za kwanza katika orodha ya shule bora zaidi nchini humo.
-
UN yataka kufunguliwa kesi ya jinai zinazofanywa dhidi ya Waislamu Myanmar
Oct 25, 2019 02:51Maafisa wawili wa Umoja wa Mataifa wametoa wito wa kufunguliwa kesi katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) ili kushughulikia jinai zinazofanywa na jeshi la Myanmar dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya katika jimbo la Rakhine nchini humo.
-
India yazidisha hatua kali za usalama kabla ya kuhitimishwa kesi ya Msikiti wa Babri
Oct 15, 2019 04:05Serikali ya India imezidisha hatua kali za usalama katika mji wa Ayodhya, jimbo la Uttar Pradesh huko kaskazini mwa nchi hiyo kabla ya kutolewa uamuzi muhimu sana wa Mahaka Kuu ya nchi hiyo juu ya mzozo wa eneo la Msikiti wa Babri linalogombaniwa baina ya Waislamu na Wahindu.
-
Waislamu Tanzania wajiandaa kufanya Maulidi ya Mtume Muhammad SAW kwa hamasa kubwa zaidi mwaka huu + Sauti
Oct 07, 2019 09:33Viongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) wametoa ufafanuzi kuhusu maandalizi ya Maulidi ya Kitaifa yanavyoendelea jijini Mwanza na wamejipanga kufanya shughuli mbalimbali za kijamii kuelekea maadhimisho hayo ya kuzaliwa Bwana Mtume Muhammad SAW. Ammar Dachi na taarifa zaidi kutoka Dar es Salaam...
-
Zarif: Iwapo Marekani inataka mazungumzo na Iran lazima itekeleze ahadi zake
Sep 29, 2019 07:16Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, Iran haitaacha mustakabali wa uchumi na wananchi wake utegemee mkutano wa kimaonyesho na Rais Donald Trump wa Marekani. Ameongeza kuwa, kama ambavyo Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu alivyosema, 'iwapo Mareknai inataka kufanya mazungumzo na Iran, ni lazima kwanza itekeleze ahadi zake na isitishe vikwazo.'
-
Hujuma dhidi ya Waislamu zimeongeza nchini Marekani katika kipindi cha uongozi wa Trump
Sep 18, 2019 07:48Baraza la Uhusiano wa Kiislamu la Marekani limetangaza kuwa, hujuma na mashambulio dhidi ya Waislamu nchini humo yameongezeka mno katika kipindi cha uongozi wa Rais Donald Trump.
-
Independent: India inafanya mikakati ya kuwapokonya uraia mamilioni ya Waislamu
Aug 20, 2019 02:35Gazeti la Independent linalochapishwa nchini Uingereza limefichua kwamba, serikali ya India inapanga mikakati ya kuwapokonya uraia watu wasiopungua milioni nne aghlabu yao wakiwa ni Waislamu na kuwatambua kuwa ni wahajiri wa kigeni.