Feb 02, 2023 02:12
Nasser Kan'ani, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, siku ya Jumatatu alijibu upayukaji mpya wa baadhi ya viongozi wa Marekani na kusema kuwa, serikali ya Washington inaelewa vilvyo kwamba Iran haiwezi kufumbia macho uchokozi wa aina yoyote ile wa ardhi yake na lazima itatoa majibu makali kwa yeyote anayelichokoza taifa hili la Kiislamu.