Hamas: Baadhi ya nchi za Kiarabu zinaichochea Israel iishambulie Gaza
https://parstoday.ir/sw/news/west_asia-i48497-hamas_baadhi_ya_nchi_za_kiarabu_zinaichochea_israel_iishambulie_gaza
Mwanachama wa ngazi ya juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) ametahadharisha kuwa baadhi ya nchi za Kiarabu zinaushawishi utawala wa Kizayuni utekeleze mashambulizi huko Ghaza.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Sep 30, 2018 23:09 UTC
  • Hamas: Baadhi ya nchi za Kiarabu zinaichochea Israel iishambulie Gaza

Mwanachama wa ngazi ya juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) ametahadharisha kuwa baadhi ya nchi za Kiarabu zinaushawishi utawala wa Kizayuni utekeleze mashambulizi huko Ghaza.

Mahmoud al Zahar amesisitiza kuwa baadhi ya  viongozi wa nchi za Kiarabu na Mahmoud Abbas Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina wanaandaa mipango ili pamoja na  kuishinikiza Hamas ibadilishane mateka, Israel iweze kutekeleza mashambulizi katika Ukanda wa Ghaza. Al Zahar hakutoa maelezo zaidi kuhusu mpango huo wa nchi za Kiarabu hata hivyo amesema kuwa baadhi ya hatua za Mahmoud Abbas kama kusitisha kuhamishia fedha katika mabenki ya Ghaza zinatekelezwa kwa lengo la kuwafanya wakazi wa eneo hilo kuwa dhidi ya Hamas. 

Mahmoud Abbas, Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina

Mamlaka ya Ndani ya Palstina imekata asilimia 50 ya mishahara ya wafanyakazi wa Ghaza ili kuiweka chini ya mashinikizo harakati ya Hamas. Si  hilo tu, mamlaka hiyo imepunguza pia mgao wa umeme na utumaji wa misaada ya kitiba katika eneo hilo. Hatua hizo za Mamlaka ya Ndani ya Palestina chini ya uongozi wa Mahmoud Abbas zimewapelekea maelfu ya Wapalestina kustaafu kwa lazima  huku ulipaji wa mishahara yao na wafanyakazi wengine ikiwa imesimamishwa kwa miezi kadhaa sasa.