Marekani yatuma maelfu ya magaidi wa Daesh barani Ulaya
Gazeti moja linalochapishwa nchini Marekani limeandika kuwa, Marekani na wapinzani nchini Syria wamewatuma katika nchi za Ulaya maelfu ya magaidi wa kundi la ukufurishaji la Daesh kutokea Syria.
Gazeti la Business Insider limefichua katika ripoti yake kuwa baada ya kupata pigo Daesh huko Iraq na Syria, maelfu ya magaidi wa kundi hilo wametoroshewa katika nchi za Ulaya kupitia Uturuki kufuatia makubaliano yaliyofikiwa kati ya Marekani na wanamgambo wanaopigana dhidi ya serikali ya Syria.
Gazeti hilo la nchini Marekani huku likiendelea kufichua kuwa, magaidi hao wanavushwa na kupelekwa Ulaya mkabala na kutoa rushwa na hongo limeandika kuwa: Mamluki wa kundi la Daesh walitoa rushwa ili kuweza kukimbilia katika nchi za Ulaya kabla ya kukombolewa mji wa Raqqah huko Syria. Marekani imekuwa na nafasi katika kueneza mgogoro na machafuko huko Syria katika kipindi cha karibu miaka saba iliyopita; ambapo Washington imeukuwa ikiyagawa makundi ya kigaidi kimakundi yaani ugaidi mbaya na mzuri huku ikiyaunga mkono kwa hali makundi hayo ya kigaidi kwa maslahi yake.
Kundi la kigaidi la Daesh katika miaka ya karibuni lilipata uungaji mkono wa kifedha na kijeshi kutoka Marekani na waitifaki wake wa Magharibi na Kiarabu ikiwemo Saudi Arabia na hivyo kufanya jinai chungu nzima katika nchi za eneo la Mashariki ya Kati hususan huko Iraq na Syria.