May 01, 2018 08:35
Ni matumaini yangu kuwa hujambo mpenzi msikilizaji popote pale ulipo. Jumatatu ya tarehe 30 Aprili ilisadifiana na siku ya mwisho ya kuondoka Wareno baada ya kutimuliwa kwenye eneo la maji ya kusini mwa Iran. Kwa mnasaba wa tukio hilo, siku hii inajulikana katika kalenda rasmi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kama "Siku ya Taifa ya Ghuba ya Uajemi". Baada ya utangulizi huo mfupi nakuomba sasa ujiweke tayari kusikiliza yale niliyokuandalia kwa mnasaba wa siku hiyo.