-
Viongozi wa Marekani wanyoosheana vidole vya lawama kuhusu kufedheheshwa nchi hiyo huko Afghanistan
Aug 20, 2021 09:19Kufuatia kuingia tena madarakani huko Afghanistan kundi la Taliban, ambayo ni ishara ya wazi ya kushindwa vibaya kijeshi nchi hiyo ya Magharibi, Rais Joe Biden amekososlewa vikali kuhusiana na siasa zake za kuondoa askari wa nchi hiyo katika ardhi ya Afghanistan, ambapo sasa vyombo tofauti vya intelijensia na usalama vya Washington vinarushiana lawama kuhusu kadhia hiyo.
-
Ripoti mpya kuhusu matokeo ya vita vya miaka 20 vya Marekani huko Afghanistan
Aug 20, 2021 00:04Taasisi ya Watson Institute for International and Public Affairs katika Chuo Kikuu cha Brown imetangaza katika ripoti yake mpya kwamba, Marekani imetumia dola trilioni 2.26 katika vita vyake vya miaka 20 huko Afghanistan ambavyo vilianza msimu wa mapukutiko wa mwaka 2001.
-
Rais wa Afghanistan aliyeikimbia nchi yuko Imarati; adaiwa kubeba dola milioni 169
Aug 19, 2021 03:43Rais aliyetoroka nchi yake ya Afghanistan Ashraf Ghani yupo katika nchi Umoja wa Falme za Kiarabu UAE. Hilo limethibitishwa na Wizara ya Mashauri ya Kigeni Imarati .
-
Taliban: Imam Hussein AS ndiye aliyejitoa mhanga mkubwa zaidi katika historia ya Uislamu
Aug 19, 2021 03:18Mkuu wa kamati ya utamaduni ya kundi la Taliban amesema, kundi hilo halina mgongano wala uadui na Mashia na akasisitiza kwamba Imam Hussein AS ndiye aliyejitoa mhanga mkubwa zaidi katika historia ya Uislamu.
-
New York Times lafichua: CIA ilimtahadharisha Biden kuhusu mgogoro utakaozuka Afghanistan
Aug 19, 2021 03:18Gazeti la New York Times limefichua kuwa, kabla wanajeshi wa Marekani hawajaondoka Afghanistan, Shirika la Ujasusi la Marekani CIA lilikuwa limeshamtahadharisha rais wa nchi hiyo Joe Biden kuhusu mgogoro utakaozuka ndani ya Afghanistan.
-
Kadhaa wauawa katika maandamano ya 'bendera' nchini Afghanistan
Aug 18, 2021 13:34Kwa akali watu watatu wameuawa huku makumi ya wengine wakijeruhiwa katika maandamano ya kulalamikia kitendo cha wapiganaji wa Taliban kuondoa bendera ya taifa hilo na kuweka bendera ya kundi hilo katika maeneo muhimu ya mji wa Jalalabad, mashariki mwa Afghanistan.
-
Shamkhani aionya Israel; Hatima ya uvamizi ni kutimuliwa
Aug 18, 2021 13:23Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran ameuonya utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kuuambia kuwa, sera yake ya uvamizi na ukaliaji ardhi za Wapalestina kwa mabavu itapatwa na hatima ya kufedhehesha kama iliyoipata Marekani huko Afghanistan.
-
Nujabaa: Afghanistan ni funzo na somo kubwa kwa vibaraka na waitifaki wa Marekani
Aug 17, 2021 15:55Msemaji wa harakati ya Nujabaa nchini Iraq amesema kuwa wanamapambano wa nchi hiyo hawataruhusu Baghdad ipatwe na hatima kama ile ya Kabul huko Afghanistan na kusisitiza kuwa hali ya sasa ya Afghanistan ni somo na ibra kwa vibaraka na waitifaki wa Marekani.
-
Kuanza duru mpya katika historia ya kisiasa ya Afghanistan
Aug 17, 2021 11:03Baada ya wanamgambo wa Taliban kudhibiti mji mmoja baada ya mwingine na hatimaye kuudhibiti mji mkuu Kabul baada ya Rais Muhammad Ashraf Ghani kuikimbia nchi, sasa kumeanza duru mpya katika historia ya kisiasa ya nchi hiyo.
-
Khatibzadeh: Iran itatumia uwezo wake kuleta maelewano Afghanistan
Aug 17, 2021 04:02Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itatumia uwezo wake wote kwa ajili ya kuhimiza mazungumzo na maelewano nchini Afghanistan.