-
Safari ya pili ya Hamad bin Isa Aal Khalifa nchini Misri katika kipindi cha chini ya miezi mitatu
Jun 10, 2017 03:56Huku mivutano na mitibuano ya Waarabu kwa Waarabu katika eneo la Ghuba ya Uajemi ikiwa imezidi kupamba moto, Mfalme wa Bahrain Hamad bin Isa Aal Khalifa, ambaye siku tatu zilizopita alifanya safari ambayo haikuwa ya kushangaza mjini Riyadh, Saudi Arabia, baada ya kupita muda wa chini ya miezi mitatu, siku ya Alkhamisi alielekea tena Cairo mji mkuu wa Misri na tab'an jana Ijumaa alikuwa mgeni wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).
-
Kituo cha Haki za Binadamu cha Bahrain chakosoa utendaji haribifu wa utawala wa Aal Khalifa
Jun 07, 2017 15:34Kituo cha Haki za Binadamu nchini Bahrain kimekosoa na kulaani utendaji wa utawala wa Kifalme wa nchi hiyo wa Aal Khalifa na kutoa wito wa kusitishwa utendaji huo haribifu.
-
Mfungamano mkubwa baina ya vitendo vya Aal Khalifa na utawala wa Kizayuni katika kukandamiza wapinzani
Jun 07, 2017 06:07Serikali ya ukoo wa Aal Khalifa nchini Bahrain inafanya jinai kubwa dhidi ya raia wa kawaida, wanaharakati na shakhsia mbalimbali wa nchi hiyo kiasi kwamba vitendo vyake hivyo havina tofauti yoyote na jinai zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina.
-
Qatar: Madai dhidi yetu si ya kweli na hayana msingi
Jun 05, 2017 07:45Baada ya Saudi Arabia, Misri, Imarati na Bahrain kukata uhusiano na Qatar mapema leo Jumatatu, wizara ya mambo ya nje wa Qatar imesema, imesikitishwa na hatua hiyo.
-
Kuongezeka hasira za Wabahrain dhidi ya Marekani
Jun 03, 2017 02:28Habari kutoka nchini Bahrain zinaonesha kuongezeka mno hasira za wananchi wa nchi hiyo dhidi ya Marekani kutokana na siasa zake za kuunga mkono ukandamizaji unaofanywa na utawala wa Aal Khalifa dhidi ya raia hususan kuendelea kuzingirwa nyumba ya Sheikh Isa Qassim kwa baraka kamili za Marekani.
-
Ghasia mpya Bahrain, Sheikh Qassim hajulikani aliko
May 29, 2017 07:11Askari wa utawala wa kiimla wa Bahrain wameendelea kuwashambulia wananchi wanaoandamana kumuunga mkono mwanazuoni wa Kiisalmu Sheikh Isa Qassim ambaye sasa ametoweka na hajulikani aliko.
-
Wasiwasi wa Umoja wa Ulaya kuhusiana na hali ya Bahrain
May 28, 2017 07:34Umoja wa Ulaya umetoa taarifa ambayo imeelezea wasiwasi wake kuhusu hali ya Bahrain na kutoa indhari kuhusiana na kuzidi kuwa mbaya hali ya nchi hiyo ya Ghuba ya Uajemi.
-
Utawala wa Aal-Khalifa wapiga marufuku watu kushiriki mazishi ya watu uliowaua
May 27, 2017 13:37Utawala wa kidikteta wa Aal-Khalifa nchini Bahrain umepiga marufu kujitokeza watu katika mazishi ya mashahidi waliouawa na askari wa utawala huo eneo la Dizar, kaskazini magharibi mwa mkoa wa Pwani wa nchi hiyo.
-
Wabahrain waendeleza maandamano ya kulaani udhalimu wa ufalme wa nchi hiyo
May 26, 2017 07:30Wananchi wa Bahrain wameendeleza maandamano ya kitaifa ya kulaani udhalimu na umwagaji damu unaoendelezwa na utawala wa Aal Khalifa katika kijiji cha Diraz ambacho ni makao ya mwanazuoni maarufu wa Kiislamu Sheikh Isa Qassim.
-
Utawala wa Aal Khalifa wapanga kuchukua hatua ya kijeuri ya kumbaidisha Sheikh Isa Qassim
May 25, 2017 07:52Utawala wa Aal Khalifa ukiungwa mkono na Saudi Arabia na Marekani umepanga kuchukua uamuzi wa kifidhuli na kijeuri wa kumbaidisha na kumpeleka uhamishoni Sheikh Isa Qassim, mwanazuoni mkubwa wa Waislamu wa madhehebu ya Shia, hatua ambayo endapo itatekelezwa itazidisha maradufu ghadhabu na hasira za wananchi wanamapinduzi wa Bahrain.