-
CAIR yaonya kuhusu kuenea chuki dhidi ya Uislamu baada ya mbunge Muislamu kutishiwa kuuawa Marekani
Apr 07, 2019 02:59Baraza la Uhusiano wa Kiislamu nchini Marekani (CAIR) limeonya kuwa vitendo vya uhalifu vinavyotokana na chuki dhidi ya Waislamu vimeongezeka nchini humo, baada ya mtu mmoja kukamatwa na kupandishwa kizimbani kwa kutishia kumuua Mbunge Muislamu katika Baraza la Wawakilishi la Marekani, Ilhan Omar.
-
Bunge la Australia lamjia juu Seneta mwenye chuki dhidi ya Waislamu
Apr 04, 2019 02:35Bunge la Australia limepiga kura kwa kishindo kupasisha hoja ya kumlaani na kumkosoa Seneta mwenye misimamo mikali wa mrengo wa kulia, kutokana na matamshi yake ya chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu baada ya shambulizi la kigaidi la mwezi uliopita nchini New Zealand.
-
Indhari ya Mkuu wa Sera za Nje wa EU kuhusu uenezaji chuki dhidi ya Uislamu
Mar 28, 2019 04:37Mashambulizi ya kigaidi ya makundi yenye kuchupa mipaka hususan magaidi wa Daesh huko barani Ulaya na Marekani yamepelekea kuandaliwa uwanja wa kushadidishwa mashambulizi ya propaganda na kuibua anga ya vita vya kisaikolojia dhidi ya dini ya Uislamu na Waislamu kwa ujumla.
-
Sisitizo la Antonio Guterres la ulazima wa kukabiliana na chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia)
Mar 24, 2019 07:37Matukio ya miaka ya hivi karibuuni katika medani ya kimataifa hususan kujitokeza makundi yenye kufurutu ada na kuenea vitendo vyao vya ugaidi katika madola ya Magharibi, yalivipatia vyombo vya habari na tawala za nchi hiyo kisingizio tosha cha kueneza chuuki dhidi ya Uislamu.
-
Wenye chuki na Uislamu Denmark waivunjia heshima Qur'ani tukufu kwa kuuchoma moto msahafu
Mar 23, 2019 08:02Katika harakati nyingine ya uenezaji chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia), kiongozi wa chama kimoja cha mrengo wa kulia chenye misimamo ya kufurutu mpaka nchini Denmark ameuchoma moto msahafu mbele ya jengo la bunge la nchi hiyo.
-
Misikiti mitano yavamiwa katika mji wa Birmingham nchini Uingereza
Mar 21, 2019 15:04Misikiti mitano imeshambuliwa katika mji wa Birmingham nchini Uingereza, wiki moja baada ya kutokea mashambulizi ya kigaidi nchini New Zealand na kuua makumi ya Waislamu na kujeruhi makumi ya wengine.
-
Guterres: Kuna udharura wa kupambana na chuki dhidi ya Uislamu duniani
Mar 16, 2019 04:45Katibu MKuu wa Umoja wa Mataifa sanjari na kulaani mashambulio ya kigaidi yaliyofanywa dhidi ya misikiti miwili katika mji wa Christchurch nchini New Zealand jana Ijumaa na kuua makumi ya watu, ametoa mwito wa kuundwa mikakati ya kupambana na chuki dhidi Uislamu zinazoenea kwa kasi katika maeneo mbalimbali ya dunia.
-
OIC: Chuki na ubaguzi dhidi ya Waislamu vilifika kileleni mwaka jana
Feb 28, 2019 16:03Kituo cha Islamophobia Watch kinachofuatilia chuki na ubaguzi unaofanyika dhidi ya Uislamu na Waislamu duniani kimetangaza kuwa, ubaguzi na chuki dhidi ya Waislamu vilifikia kileleni mwishoni mwa mwaka uliopita wa 2018.
-
Iran na Uturiki zahimizwa kukabiliana na ugaidi na propaganda chafu dhidi ya Uislamu
Dec 05, 2018 08:09Mkuu wa Jumuiya ya Masuala ya Dini nchini Uturuki amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Uturuki ambazo ni nchi kubwa zaidi katika eneo la Mashariki ya Kati zinapaswa kuzidisha ushirikiano kwa ajili ya kupambana na ugaidi na njama zinazoeneza propaganda za kuchafua sura safi ya Uislamu.
-
Waislamu Canada wataka 'Siku ya Kitaifa ya Kupambana na Chuki dhidi ya Uislamu'
Nov 23, 2018 07:52Waislamu nchini Canada wamesema jinai zinazotokana na chuki dhidi ya Uislamu zimeshtadi huku wakiitaka serikali izindue mpango mkakati wa kuziunganisha jamii za nchi hiyo.