-
Rezai: Hatua yoyote ya kijeshi itakayochukua Marekani Iraq ni sawa na shambulio linalofanywa na DAESH (ISIS)
Mar 31, 2020 11:23Katibu wa Halmashauri ya Kuainisha Maslahi ya Mfumo wa Kiislamu wa Iran amesema, hatua yoyote ya kijeshi itakayochukua Marekani nchini Iraq itakuwa sawa na hujuma inayofanywa na kundi la kigaidi na ukufurishaji la DAESH (ISIS).
-
Hashdu Sha'abi yatekeleza operesheni ya mafanikio katika mikoa minne ya Iraq
Feb 29, 2020 23:11Kamandi ya Harakati ya Wananchi ya Hashdu sh-Sha'abi ya Iraq imetangaza kumalizika kwa operesheni ya mafanikio makubwa dhidi ya magaidi katika mikoa minne ya Al-Anbar, Diyala, Kirkuk na Salahdin.
-
Hatua ya kukurupuka ya Marekani ya kumuwekea vikwazo Katibu Mkuu wa Kataeb Hizbullah ya Iraq
Feb 28, 2020 02:05Marekani imetuma idadi kubwa ya wanajeshi wake huko Iraq tangu mwaka 2014 kwa kisingizio cha kupambana na kundi la Daesh. Katika hatua yake ya kukurupuka Marekani imeliorodhesha jina la kiongozi wa mojawapo ya makundi muhimu ya taasisi ya Kataeb Hizbullah ya Iraq licha ya nafasi muhimu ya kundi la kujitolea la wananchi la al Hashd al Shaabi katika kutoa pigo na kuliangamiza kundi la kigaidi la Daesh huko Iraq.
-
Misri yawahukumu watu kadhaa kifungo cha maisha jela kwa kujiunga na Daesh
Jan 28, 2020 04:41Mahakama Cairo nchini Misri imewahukumu watu wasiopungua 37 vifungo mbalimbali vya jela kikiwemo kifungo cha maisha baada ya kupatikana na hatia ya kujiunga na kuliunga mkono genge la uhalifu lenye mfungamano na kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh.
-
Ujerumani yatahadharisha kuhusu kuanza tena mashambulizi ya kundi la Daesh
Jan 24, 2020 23:43Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani ametahadharisha kuwa, kuna uwezekano kundi la kigaidi la Daesh likaanza tena kutekeleza vitendo vyake vya kigaidi.
-
"ISIS walitaka kushambulia ubalozi wa Marekani Lebanon na kuisingizia Hizbullah"
Jan 24, 2020 02:45Gazeti la al Jamhuriyyah la Lebanon limefichua kuwa, genge la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) lilikuwa limepanga njama za kushambulia ubalozi wa Marekani mjini Beirut ili kuibebesha lawama harakati ya Kiislamu ya nchi hiyo Hizbullah hasa baada ya Marekani kumuua kigaidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds, cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH.
-
Mufti 'tipwatipwa' wa DAESH mwenye uzito wa kilo 245 atiwa nguvuni mjini Mosul, Iraq
Jan 18, 2020 10:37Vikosi vya usalama vya Iraq vimemtia nguvuni Abu Abdul Bari, mufti wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la DAESH (ISIS) katika mji wa Mosul, kaskazini mwa nchi hiyo. Abu Abdul Bari ni maarufu kwa utoaji fatua za kuwafanya wanawake watumwa, za ubakaji, utesaji na uangamizaji wa kimbari.
-
TV ya Saudia yamtimua mtangazaji wa Palestina kwa kutangaza mshikamano na Wayemen
Jan 14, 2020 01:00Televisheni ya Saudi Arabia imemsimamisha kazi mtangazaji wake baada ya kubainika kwamba, amekuwa akituma ujumbe katika mtandao wa kijamii wa Twitter akitangza mshikamano wake na Wayemen na kulaani mashambulizi yanayofanywa na utawala wa Riyadh dhidi ya raia wasio na hatia wa Yemen.
-
Ngome kubwa ya ISIS yaharibiwa kaskazini mwa Iraq
Jan 12, 2020 08:43Vikosi vya Kujitolea vya Wananchi wa Iraq maarufu kama Al Hashd al Shaabi vimeharibu pango kubwa zaidi la magaidi wa ISIS (Daesh) kaskazini mwa Iraq.
-
Watu 30 wauawa katika mripuko wa bomu nchini Nigeria
Jan 07, 2020 04:36Kwa akali watu 30 wameuawa huku makumi ya wengine wakijeruhiwa katika mripuko wa bomu uliotokea karibu na daraja lenye shughuli nyingi katika jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa Nigeria.