-
Ndege za kivita za Marekani zawasaidia makamanda wa Daesh Syria
Jun 25, 2018 23:51Ndege za kivita za muungano eti wa kimataifa dhidi ya kundi la kigaidi la Daesh unaoongozwa na Marekani zimewasafarisha makamanda wawili wa kundi la kigaidi la Daesh kutoka eneo a Tuimin hadi katika kituo cha Marekani kilichoko katika mji wa al Shaddadah mkoani Hasakah nchini Syria.
-
Taleban: Helikopta za Marekani zinawasaidia wanachama wa Daesh dhidi yetu
Jun 22, 2018 21:53Kundi la kigaidi la Taleban nchini Afghanistan limesema kwamba helikopta za kijeshi za Marekani zimekuwa zikiwasaidia wanachama wa kundi la kigaidi la Daesh (ISIS) katika uwanja wa vita kati ya wanachama wa makundi hayo sambamba na kushambulia ngome za Taleban katika mkoa wa Nangarhar, mashariki mwa nchi hiyo.
-
Harakati ya Nujabaa: Daesh ni mradi wa Marekani kwa ajili ya kufikia malengo yake
Jun 10, 2018 12:18Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama ya Nujaba ya nchini Iraq amesema kuwa, kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) ni njia nzuri ya Marekani kwa ajili ya kufikia malengo yake ya kikoloni na kiuchumi kupitia kisingizio cha kupambana na ugaidi katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Vitisho vya DAESH vyasababisha skuli zote za wasichana kufungwa katika jimbo la Nangarhar, Afghanistan
Jun 05, 2018 09:21Idara ya Elimu na Mafunzo ya jimbo la Nangarhar mashariki mwa Afghanistan imetangaza kuwa skuli za wasichana jimboni humo zinafungwa kuanzia leo kufuatia vitisho vya mashambulio ya kigaidi vilivyotolewa na kundi la ukufurishaji la DAESH (ISIS).
-
Gaidi wa Daesh anayehusika na utegaji mabomu anaswa nchini Iraq
Jun 02, 2018 08:59Kituo cha Uchunguzi cha Harakati ya Muqawama wa Kiislamu Nujaba, kimetangaza habari ya kutiwa mbaroni gaidi wa ngazi ya juu katika genge la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) akiwa pamoja na watu wengine watano.
-
Iran kuishtaki Marekani kwa kutumia ushahidi wa Trump
May 30, 2018 03:40Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inajiandaa kuishtaki Marekani kwa kushiriki kwa njia isiyo ya moja kwa moja katika mashambulizi ya kigaidi ya mwaka jana hapa nchini, kwa kutumia ushahidi wa Rais Donald Trump.
-
Waziri Mkuu wa Iraq atoa amri ya kufuatiliwa magaidi wa Daesh nje ya mipaka ya Iraq
May 22, 2018 23:01Waziri Mkuu wa Iraq amesisitizia ulazima wa kudhaminiwa usalama wa mipaka ya nchi hiyo na kufanyika operesheni dhidi ya wafuasi wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) nje ya mipaka ya Iraq.
-
Ndege za Marekani zashuhudiwa zikiwatumia silaha mabaki ya Daesh (ISIS) nchini Syria
May 19, 2018 09:46Kwa mara nyingine wanachama wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) wamepewa msaada wa silaha na askari wa Marekani na kuwawezesha kuingia eneo la wazi la kusini magharibi mwa jimbo la Deir ez-Zor nchini Syria.
-
Magaidi wa genge la Daesh na Jaishul-Hur washambuliana vikali kusini mwa Syria
May 14, 2018 22:11Magaidi wa makundi ya ukufurishaji ya Daesh (ISIS) na kundi la Jeishul-Hur (Jeshi huru), wameshambuliana vikali magharibi mwa mkoa wa Daraa, nchini Syria na kusababisha maafa makubwa kati yao.
-
Iran: Daesh ni silaha ya Marekani dhidi ya usalama wa Mashariki ya Kati
May 13, 2018 03:12Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelitaja kundi la kigaidi na kitakfri la Daesh (ISIS) kama chombo cha Marekani na madola mengine ya kibeberu cha kuvuruga usalama katika eneo hili la Mashariki ya Kati.