-
Waziri Mkuu wa Ethiopia amjibu Trump anayelilia Tuzo ya Nobel
Jan 15, 2020 23:02Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed amejibu matamshi ya Rais Donald Trump wa Marekani aliyedai hivi karibuni kuwa yeye ndiye aliyepaswa kupewa Tuzo ya Amani ya Nobel mwaka jana 2019 na kusisitiza kuwa, Trump anapaswa kuwasilisha malalamiko yake kwa Kamati Andalizi ya Tuzo ya Nobel na sio kwa taifa hilo la Pembe ya Afrika.
-
Mazungumzo kuhusu bwawa la al-Nahdha yavunjika nchini Ethiopia
Jan 11, 2020 01:20Wizara ya Maji ya Misri imetangaza kuwa, mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea huko Addis Ababa kati ya nchi hiyo, Ethiopia na Sudan kuhusiana na bwawa na al-Nahdha yamevunjika baada ya pande husika kushindwa kufikia makubaliano.
-
Viongozi wa Kiislamu Ethiopia walaani hujuma dhidi ya misikiti Amhara
Dec 25, 2019 03:54Viongozi wa Kiislamu nchini Ethiopia wamelaani vikali hujuma na kuteketezwa moto misikiti minne katika jimbo la Amhara ambalo liko kaskazini mwa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Ethiopia yarusha satalaiti yake ya kwanza katika anga za mbali
Dec 20, 2019 08:13Ethiopia leo Ijumaa imerusha satalaiti yake ya kwanza katika anga za mbali na kujiunga na nchi kadhaa za Kiafrika ambazo zina miradi ya anga za mbali kwa malengo ya ustawi na sayansi.
-
Kamati ya Nobel: Waziri Mkuu wa Ethiopia anapasa kuzungumza na vyombo vya habari wakati wa kupokea tuzo ya amani
Dec 06, 2019 11:45Abiy Ahmed Waziri Mkuu wa Ethiopia hatozungumza na vyombo vya habari wiki ijayo atakapokuwa mjini Oslo kupokea tuzo ya Amani ya Nobl; hatua iliyompelekea kukosolewa na kamati ya tuzo hiyo ambayo imesema kuwa uhuru wa vyombo vya habari una umuhimu.
-
Jubaland: Majeshi ya Ethiopia na Somalia yanataka kumpindua Rais Madobe
Nov 17, 2019 04:16Serikali ya eneo lenye mamlaka ya ndani la Jubaland, Kusini mwa Somalia imedai kuwa wanajeshi wa Ethiopia wanakula njama za kumpindua Rais Ahmed Madobe wa jimbo hilo.
-
Ethiopia yapinga upatanishi wa Marekani katika mazungumzo ya bwawa la El Nahdha
Nov 09, 2019 23:14Ujenzi wa bwawa la El Nahdha na suala la kugawana manufaa ya maji ya Mto Nole kati ya nchi za Misri, Ethiopia na Sudan limegeuka na kuwa mgogoro kati ya nchi hizo tatu hususan Misri na Ethiopia kwa kadiri kwamba Cairo imewasilisha pendelezo la usuluhishi kutoka nje baada ya kukwama mazungumzo baina ya pande husika.
-
Ethiopia yakataa upatanishi wa Marekani katika mgogoro wa bwawa na El Nahdha
Nov 08, 2019 11:45Serikali ya Ethiopia imetangaza kuwa, haikubali upatanishi wa Marekani katika mazungumzo yanayohusiana na ujenzi wa Bwawa na El Nahdha juu ya maji ya Mto Nile.
-
Abiy Ahmed: Watu 86 wameuawa katika machafuko ya karibuni Ethiopia
Nov 04, 2019 23:22Waziri Mkuu wa Ethiopia amesema kuwa, watu 86 wameuawa katika maandamano ya kupinga serikali yaliyotokea mwezi uliopita nchini humo.
-
Serikali ya Ethiopia: Watu 78 wameuawa katika maandamano, idadi inaweza kuongezeka
Nov 01, 2019 04:38Serikali ya Ethiopia imetangaza kuwa watu wasiopungua 78 waliuawa katika maandamano ya upinzani ya kupinga muamala mbaya dhidi ya mwanaharakati mwenye ushawishi mkubwa, ambaye pia ni mjasiriamali wa vyombo vya habari nchini humo.