-
Jenerali Mzayuni akiri nguvu za makombora za HAMAS huko Palestina
Apr 29, 2019 23:42Jenerali mmoja Mzayuni amekiri kuwa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS ina nguvu kubwa za makombora ambazo zinaweza kusambaratisha maisha ya wakazi wa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Hamas: Mamlaka ya Ndani ya Palestina sio mwakilishi wa Wapalestina
Apr 17, 2019 09:51Mahmoud al-Zahar, mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas amesema kuwa, Mamlaka ya Ndani ya Palestina sio mwakilishi wa Wapalestina.
-
Hamas: Serikali mpya ya Abbas itasahilisha utekelezaji wa "Muamala wa Karne"
Apr 14, 2019 02:56Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imekosoa uundwaji wa serikali mpya Palestina inayotawaliwa na wanachama wa chama chake cha Fath, ikisisitiza kuwa serikali ya namna hiyo itawepesisha utekeleza wa njama za Marekani dhidi ya Wapalestina zilizopewa jina "Muamala wa Karne".
-
Israel: Harakati ya HAMAS inao uwezo wa kuingia Israel na kuua askari wetu wengi
Mar 11, 2019 04:33Waziri wa Elimu na Mafunzo wa Utawala Haramu wa Kizayuni wa Israel, Naftali Bennett amekiri uwezo mkubwa wa kijeshi wa Harakati ya Kiislamu ya Palestina HAMAS.
-
Harakati ya Hamas yakosoa siasa za Rais Mahmoud Abbas
Feb 25, 2019 23:08Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kuwa, Rais Mahmoud Abbas wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina anakubaliana na mpango wa Marekani wa "Muamala wa Karne" lakini viongozi wa Fat'h wanataka kumuonyesha kiongozi huyo kwamba, anaupinga mpango huo.
-
HAMAS: Taifa la Palestina limethibitisha kwamba, Masjidul Aqswa ni mstari mwekundu
Feb 23, 2019 04:02Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imetangaza kuwa, msikiti wa al-Aqswa ni mstari mwekundu wa Umma wa Kiislamu.
-
Hamas: Kujiuzulu kamanda wa makomandoo wa Israel ni ishara ya nguvu ya Wapalestina
Feb 20, 2019 04:36Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amesema kujiuzulu kamanda wa vikosi maalumu vya makomandoo wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel baada ya kushindwa na Wapalestina katika oparesheni ya Khan Yunus ni ishara ya nguvu kubwa za harakati za kupigania ukombozi Palestina au muqawama na kusambaratika mahesabu ya wakuu wa utawala wa Kizayuni.
-
Mpalestina afa shahidi gerezani Israel baada ya kunyimwa matibabu
Feb 07, 2019 03:51Mfungwa Mpalestina amekufa shahidi akiwa katika gereza la utawala wa Kizayuni wa Israel baada ya kunyimwa matibabu.
-
HAMAS yakaribisha kufanyika uchaguzi mkuu wa Palestina katika ngazi zote
Jan 26, 2019 23:07Mjumbe mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesisitizia kufanyika uchaguzi wa Palestina katika ngazi zote ukiwemo wa Bunge, Rais wa Mamlaka ya Ndani na Baraza la Taifa.
-
HAMAS yasisitizia kuundwa muungano wa nchi zinazoihami Palestina
Jan 18, 2019 00:24Mahmoud Az-Zahar, mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema, adui wa Lebanon, Syria na Gaza ni utawala ghasibu wa Kizayuni tu; na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni muungaji mkono wa wanamapambano wa muqawama.