-
Jihadul-Islami na HAMAS zalaani hatua ya Ujerumani dhidi ya Hizbullah ya Lebanon
May 02, 2020 03:30Harakati ya Jihadul-Islami ya Palestina imelaani hatua ya Ujerumani ya kuiweka Hizbullah ya Lebanon kwenye orodha ya makundi ya kigaidi na kueleza kwamba hatua hiyo inadhihirisha upendeleo na uungaji mkono wa Berlin kwa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel.
-
Hizbullah ya Lebanon yasisitiza mapambano dhidi ya ufisadi na ubeberu wa sarafu ya dola
Apr 30, 2020 12:23Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya nchini Lebanon imetoa taarifa ikisema kuwa, mapambano dhidi ya ufisadi na kuzuia ubeberu wa sarafu ya Dola ya Marekani kwenye uchumi wa nchi, ni jambo la dharura.
-
Harakati ya Hizbullah ya Lebanon: Muqawama uko katika kilele cha uwezo na nguvu
Apr 13, 2020 07:59Mjumbe wa Baraza Kuu la Harakati ya Muqawama wa Hizbullah nchini Lebanon ameeleza katika kumbukumbu za shambulio la mwaka 1996 la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel katika eneo la kusini mwa Lebanon, kwamba vikwazo vya Marekani na vitisho vya utawala wa Kizayuni havijaweza kuzuia mafanikio ya muqawama.
-
Sayyid Hassan Nasrullah: Kukabiliana na Marekani ni lazima kuwe kwa pande zote na kuhusishe sekta zote
Feb 16, 2020 16:06Katibu Mkuu wa Harakati ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa Marekani ni muhusika wa vita vyote eneo la Asia Magharibi na amesisitiza kuwa, ni lazima kuendesha muqawama katika pande zote kukabiliana na utawala huo wa kibeberu wa Marekani.
-
"ISIS walitaka kushambulia ubalozi wa Marekani Lebanon na kuisingizia Hizbullah"
Jan 24, 2020 06:15Gazeti la al Jamhuriyyah la Lebanon limefichua kuwa, genge la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) lilikuwa limepanga njama za kushambulia ubalozi wa Marekani mjini Beirut ili kuibebesha lawama harakati ya Kiislamu ya nchi hiyo Hizbullah hasa baada ya Marekani kumuua kigaidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds, cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH.
-
Hizbullah: Maelfu ya Maqassim Soleimani watalipiza kisasi cha damu yake
Jan 16, 2020 07:58Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon ametangaza kuwa, adui asijidanganye kwamba, kwa kumuua Luteni Jenerali Qassim Soleimani njia ya mwanamapambano huyo haitaendelea, bali maelfu ya watu mfano wake watajitokeza kulipiza kisasi cha damu yake.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Lebanon aunga mkono misimamo ya Hizbullah
Dec 17, 2019 12:42Waziri wa Mambo ya Nje wa Lebanon Gebran Bassil ameunga mkono misimamo ya harakati ya muqawama ya Hizbullah katika uga wa kisiasa na kijeshi wa nchi hiyo.
-
Hizbullah yapinga masharti ya Marekani kwa ajili ya kuundwa serikali mpya ya Lebanon
Nov 26, 2019 08:02Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imepinga masharti yaliyotolewa na Marekani kwa ajili ya kuundwa serikali mpya ya Lebanon.
-
Sayyid Hassan Nasrullah: Maadui wamejawa hofu kwa kushuhudia matembezi ya Arubaini
Oct 19, 2019 13:36Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon Sayyid Hassan Nasrullah amesisitiza kuwa, uwepo wa mamilioni ya watu mjini Karbala ni jambo lisilo na mfano katika historia na kwamba Marekani, utawala haramu wa Kizayuni, mabeberu na madhalimu wa dunia wanahisi hofu kubwa kwa kushuhudia matembezi ya mamilioni ya watu katika Arubaini ya Imam Hussein (as).
-
Hizbullah: Hatutosalimu amri mbele ya mashinikizo ya Marekani
Oct 10, 2019 12:07Naibu Mkuu wa Baraza la Utendaji la Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesisitiza kuwa vikwazo vya Marekani haviwezi kudhoofisha imani na ahadi yake ya kulinda nchi na raia.