-
Aoun atetea oparesheni ya Hizbullah dhidi ya utawala wa Kizayuni
Oct 02, 2019 08:05Rais wa Lebanon amekutana na Mjumbe wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Lebanon na kutetea oparesheni iliyofanywa na harakati ya Hizbullah ya nchi hiyo dhidi ya chokochoko za utawala wa Kizayuni.
-
Sheikh Nabil Qaouk: Vikwazo vya Marekani havijawa na taathira yoyote kwa Hizbullah
Sep 29, 2019 02:29Mjumbe wa Baraza la Utendaji la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amesisitiza kuwa, vikwazo vya Marekani dhidi ya harakati hiyo havijawa na taathira na kwamba, vikwazo hivyo ni matokeo ya kukata tamaa Washington.
-
Lebanon yapongeza hatua ya harakati ya Hizbullah ya kulinda nchi dhidi ya Israel
Sep 21, 2019 12:08Waziri wa Mambo ya Nje wa Lebanona sambamba na kubainisha kwamba siasa za serikali ya Beirut ni kujiepusha na aina yoyote ya vita katika eneo, amepongeza hatua ya harakati ya Kiislamu ya Hizbullah ya kulinda nchi hiyo mkabala na shambulio la hivi karibuni la ndege zisizo na rubani za utawala haramu wa Kizayuni.
-
Sayyid Hassan Nasrullah: Vita vyovyote dhidi ya Iran vina maana ya kufutwa Israel katika uso wa dunia
Sep 10, 2019 12:41Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema mbele ya mjumuiko mkubwa wa Waislamu waliofurika kwa ajili ya maombolezo ya Siku ya Ashura ya kukumbuka kuuawa shahidi Imam Husain AS kwamba, vita vyovyote vile dhidi ya Iran vitakuwa na maana ya kuangamizwa na kufutwa katika uso wa dunia, dola pandikizi la Israel.
-
Nasrullah: Hizbullah na Iran haziwezi kuyumbishwa na mashinikizo
Sep 10, 2019 07:17Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema harakati hiyo ya muqawama na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zitaendelea kusimama kidete dhidi ya mashinikizo na vikwazo vya Marekani.
-
Israel yakiri, Hizbullah imetungua ndege yake isiyo na rubani
Sep 09, 2019 11:26Duru zenye mfungamano na utawala wa Kizayuni wa Israel zimethibitisha kuwa, wapiganaji wa Hizbullah ya Lebanon wametungua ndege isiyo na rubani ya utawala huo.
-
Wazayuni wakiri: Askari watano wa Israel waliuawa ndani ya gari lililoripuliwa na Hizbullah
Sep 04, 2019 02:41Gazeti la Kizayuni la Haaretz limekiri kuwa askari watano wa Israel walikuwemo ndani ya gari la kijeshi lililoripuliwa na wanamuqawama wa Hizbullah ya Lebanon.
-
Ripota wa UN: Matatizo ya ukosefu wa amani Nigeria yapewe mazingatio
Sep 03, 2019 08:07Ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa matatizo ya kiusalama ya Nigeria yametengeneza mgogoro ambao unahitajia kupewa mazingatio haraka iwezekanavyo, la sivyo utasababisha ukosefu wa usalama katika nchi nyingine za Kiafrika.
-
"Israel haina uwezo wa kukabiliana na wanamapambano wa Kiislamu"
Sep 02, 2019 07:42Mtandao maarufu wa habari unaotembelewa na watu wengi nchini Ugiriki umetoa ripoti maalumu na kusema kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel hauna uwezo wa kukabiliana na wanamapambano wa Kiislamu wa Hizbullah ya Lebanon.
-
Al Manar: Kamanda wa jeshi la utawala wa Kizayuni aangamizwa kwenye oparesheni ya Hizbullah ya Lebanon
Sep 01, 2019 17:16Televisheni ya al Manar imetangaza kuwa harakati ya Hizbullah ya Lebanon imeangamiza moja ya zana za kijeshi za Israel katika barabara ya al Thakna katika mji wa mpakani wa Israel wa Avivim na kumuua kamanda wa kikosi kimoja wa jeshi la utawala wa Kizayuni huko kaskazini mwa ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu katika oparesheni iliyotekelezwa na harakati ya Hizbullah.