-
Mkuu wa zamani wa Mossad akiri Israel haiwezi kukabiliana na teknolojia ya makombora ya Hizbullah
Sep 09, 2018 02:21Naibu Mkuu wa zamani wa Shirika la Kijasusi la Utawala wa Kizayuni wa Israel, Mossad, amesema Harakati ya Hizbullah ya Lebanon hivi karibuni imepata mfumo mpya wa kuongoza makombora kwa kutegemea mfumo wa GPS na hivyo kubadilisha makombora yake kuwa yenye ustadi mkubwa.
-
Hizbullah: Kukombolewa Idlib kutapiku turufu ya mwisho ya Marekani, Israel na Saudia nchini Syria
Sep 03, 2018 07:54Naibu Mkuu wa Baraza la Utendaji la Hizbullah ya Lebanon amesema, kukombolewa mkoa wa Idlib kaskazini magharibi mwa Syria ambayo ni ngome ya mwisho ya magaidi katika nchi hiyo litakuwa pigo kubwa kwa Magharibi, Marekani, utawala wa Kizayuni wa Israel na Saudi Arabia.
-
Syria yaitaka Hizbullah iendelee kubakia nchini humo
Aug 26, 2018 02:25Serikali ya Syria imeitaka Harakati ya Kiislamu ya Hizbullah ya nchini Lebanona iendelee kubakisha wapiganaji wake nchini humo, baada ya kumalizika mapigano ya kijeshi kaskazini mwa nchi.
-
Bashar al-Assad alilikataa pendekezo la Saudia la kujengwa upya Syria kwa kuvunja uhusiano na Iran na Hizbullah
Aug 23, 2018 01:39Mbunge wa harakati ya Hizbullah katika bunge la Lebanon amesema, rais wa Syria hakulikubali pendekezo la Saudi Arabia la kuijenga upya nchi hiyo mkabala wa Syria kuvunja uhusiano wake na Hizbullah na Iran.
-
Hizbullah kwa mara ya kwanza imezindua aina mbalimbali za makombora yake
Aug 19, 2018 15:21Harakati ya Hizbullah ya Lebanon kwa mara ya kwanza ilipanga kuzindua leo Jumapili sehemu ya makombora yaliyotumiwa na harakati hiyo ya muqawama wa Kiislamu kwa ajili ya kuilinda nchi hiyo katika miaka ya karibuni.
-
Hizbullah: Marekani imehusika katika jinai ya mauaji ya mji wa As-Suwayda, Syria
Jul 26, 2018 14:10Harakati ya Hizbullah nchini Lebanon imetoa taarifa ikisema kuwa, harakati za makundi ya kigaidi katika eneo la al-Tanf ni hatari kubwa na kwamba Marekani imeshiriki katika jinai kubwa dhidi ya raia wa mji wa As-Suwayda kusini mwa Syria.
-
Hizbullah yalaani sera mpya ya ubaguzi wa rangi ya utawala haramu wa Israel
Jul 21, 2018 07:22Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imetoa taarifa kuhusu sheria mpya ya utawala wa Kizayuni wa Israel inayojulikana kama 'Nchi ya Kiyahudi' na kusema hiyo ni njama ya Kuyahudisha kikamilifu ardhi zote za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala huo.
-
Hizbullah: Shambulizi lolote la Israel dhidi ya Lebanon litajibiwa kwa kuteketeza eneo la Golan
Jul 03, 2018 07:35Harakati ya Hizbullah ya nchini Lebanon sambamba na kuashiria onyo kali lililotolewa na Ufaransa kwa utawala haramu wa Kizayuni, imesema kuwa chokochoko yoyote ya Israel itakayofanywa dhidi ya Lebanon, itapelekea kuteketezwa eneo la milima ya Golan inayodhibitiwa na Israel kwa sasa.
-
Hizbullah: Tuko imara zaidi hivi sasa kukabiliana na chokochoko zozote zile
Jun 25, 2018 02:56Naibu wa Mkuu wa Baraza la Utendaji la Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, harakati hiyo ya Kiislamu iko imara zaidi hivi sasa kuliko wakati mwingine wowote na kuongeza kuwa, sasa hivi Lebanon ina usalama wa kiwango cha juu zaidi katika eneo hili kutokana na ushujaa na kujitoa muhanga wanamapambano wa Kiislamu katika kukabiliana na Israel na magenge ya wakufurishaji.
-
Hizbullah: Mipango yote ya Marekani, Israel na Saudia itafeli
Jun 17, 2018 01:33Mjumbe wa Baraza Kuu la harakati ya Hizbullah ya Lebanon, Nabil Qaouk amesema kuwa, mipango ya pamoja ya Marekani, utawala haramu wa Israel na Saudi Arabia itaishia kushindwa.