-
Saudia na Imarati kushiriki mkutano wa Marekani dhidi ya Palestina
May 22, 2019 21:58Tawala vibaraka za Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu zimetangaza kuwa zitashiriki mkutano wa Marekani wa kuzindua hatua ya mwanzo ya utekelezaji wa 'Muamala wa Karne' mwezi ujao wa Juni nchini Bahrain.
-
Jamhuri ya Kiislamu yataka kuwekwa wazi kiundani tukio la bandari ya Fujairah nchini Imarati
May 13, 2019 09:49Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, Tehran imesikitishwa na matukio ya jana Jumapili yaliyotokea dhidi ya meli kadhaa za mafuta katika Bahari ya Oman katika eneo la Umoja wa Falme za Kiarabu na imetaka kuwekwa wazi na kwa kina uhakika wa matukio hayo.
-
Somalia yasambaratisha mtandao wa majasusi wa UAE
May 11, 2019 08:25Wakuu wa Somalia wametangaza kuusambaratisha mtandao wa majasusi ambao walikuwa wakiutumikia utawala wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).
-
Kuongezeka mvutano kati ya Imarati na serikali iliyojiuzulu ya Yemen
May 10, 2019 03:12Umoja wa Falme za Kiarabu, Imarati, ambayo iko katika muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia katika vita vyake vya kivamizi dhidi ya Yemen, imeingia katika mvutano mkubwa kati yake na serikali iliyojiuzulu ya Yemen ambayo hivi sasa ingali inadhibiti eneo la kusini mwa nchi hiyo.
-
UN: Yumkini Imarati imehusika katika mashambulizi ya Libya
May 07, 2019 03:26Jopo la Wataalamu wa Umoja wa Mataifa linatathmini mashambulizi ya makombora dhidi ya mji mkuu wa Libya, Tripoli, sanjari na kuchunguza uwezekano wa kutumika ndege zisizo na rubani 'drone' za Umoja wa Falme za Kiarabu katika hujuma hizo.
-
Mwanamke mwenye saratani afia gerezani Imarati licha ya indhari ya UN
May 05, 2019 09:49Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limeripoti kuwa, mwanamke aliyekuwa anaugua ugonjwa wa saratani amepoteza maisha akiwa gerezani katika Umoja wa Falme za Kiarabu, miezi miwili baada ya Umoja wa Mataifa kutoa mwito wa kuachiwa huru mwanamke huyo kwa misingi ya kwenda kupatiwa matibabu.
-
Kikao cha pande nne cha London na uungaji mkono juu ya kudumishwa vita vya Yemen
Apr 29, 2019 23:32Tokea mwezi Machi 2015 Saudi Arabia ikishirikiana na Umoja wa Falme za Kiarabu, Imarati, zimekuwa zikiendesha vita vya kidhalimu dhidi ya watu wa Yemen. Marekani na Uingereza pia zimekuwa na mchango mkubwa katika vita hivyo kwa kuzipa nchi mbili hizo za Kiarabu msaada mkubwa wa kilojistiki, habari za siri na kijeshi.
-
Ndege za kivita za kigeni zimehusika katika mashambulio ya Tripoli
Apr 29, 2019 01:51Waziri wa Mambo ya Ndani wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya amesema kuwa ndege za kigeni zilishiriki katika mashambulio ya hivi karibuni katika mji mkuu wa nchi hiyo Tripoli.
-
Netanyahu aipongeza Imarati kwa kuialika Israel katika Maonyesho ya Dubai
Apr 26, 2019 22:10Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel ameupongeza Umoja wa Falme za Kiarabu kwa kuualika utawala huo haramu kushiriki katika Maonyesho ya Dubai ya 2020.
-
Reuters: Marekani na Ulaya 'zinaiba dhahabu Afrika' kupitia Imarati
Apr 24, 2019 23:50Uchunguzi uliofanywa na shirika la habari la Reuters umefichua kuwa, tani za dhahabu zenye thamani ya mabilioni ya dola zinasafirishwa kila mwaka kwa njia za magendo kutoka Afrika kuelekea Marekani na nchi za Ulaya, huku Umoja wa Falme za Kiarabu ukitajwa kuwa lango kuu la biashara hiyo haramu.