-
Matokeo ya Mkutano wa Istanbul kati ya Iran na Troika ya Ulaya
Jul 26, 2025 12:40Suala la kuondoa vikwazo na kutilia mkazo haki ya Iran ya kurutubisha urani ni miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa katika ajenda ya "Mkutano wa Istanbul." Pande hizo zimesisitiza udharura wa kuendeleza mazungumzo.
-
Wanafunzi wa Iran washinda medali tano katika Mashindano ya Kimataifa ya Fizikia 2025
Jul 26, 2025 02:31Timu ya wanafunzi wa shule za upili kutoka Iran imejinyakulia medali tano za fedha katika Mashindano ya 55 ya Kimataifa ya Fizikia (International Physics Olympiad - IPhO 2025) yaliyofanyika jijini Paris, Ufaransa.
-
Helikopta ya Jeshi la Wanamaji la Iran yaitimua manowari ya US katika Bahari ya Oman
Jul 24, 2025 06:55Helikopta ya Jeshi la Wanamaji la Iran imeitimua manowari ya mashambulizi ya Marekani iitwayo USS Fitzgerald katika Bahari ya Oman, kwa kutoa ishara za onyo na hatimaye kuilazimisha ibadili mkondo wake kuelekea upande wa kusini wa eneo hilo.
-
Iran yaalani ukatili mkubwa wa sera ya njaa na mauaji ya Israel dhidi ya wakazi wa Gaza
Jul 23, 2025 11:07Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani " ukatili mkubwa" unaofanywa na utawala ghasibu wa Israel, na kulaani sera ya njaa na mauaji ya utawala huo dhidi ya Wapalestina wanaotafuta misaada huko Gaza.
-
Rais Pezeshkian: Ziitwazo ‘haki za binadamu’ na ‘asasi za kimataifa’ si chochote ila ni uwongo tu
Jul 22, 2025 13:55Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, zinazoitwa haki za binadamu na asasi za kimataifa si chochote zaidi ya uwongo tu na akabainisha kwamba, katika dunia ya leo iliyostaarabika na mbele ya macho ya watu wote, wanawakatia maji na chakula watu wanyonge, wanawake na watoto na kufanya mauaji ya kimbari; kisha wanazungumzia haki za binadamu, huku wao wenyewe wakiwa wamekiuka vipimo vyote vya kimataifa na haki za binadamu na kufanya jinai dhidi ya ubinadamu kila mahali dunian
-
Iran, Uturuki: Ulimwengu wa Kiislamu uchukue hatua dhidi ya mauaji ya kimbari yanayofanywa na Israel Ghaza
Jul 22, 2025 11:06Mawaziri wa mambo ya nje wa Iran na Uturuki wametoa wito kwa mataifa ya Kiislamu duniani kuchukua hatua kali za kusaidia kukomesha vita vya miezi 21 vya mauaji ya kimbari vinavyoendelezwa na utawala wa kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Ghaza.
-
Iran yatilia shaka 'hadhi' ya Tuzo ya Nobel baada ya Trump 'kuteuliwa'
Jul 22, 2025 06:43Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran, Esmaeil Baqaei ametilia shaka itibari na uhalisi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, akisema tuzo hiyo yenye heshima kubwa zaidi ya amani duniani, imegeuzwa na kuwa chombo cha kisiasa badala ya kuwa nembo ya amani kwa wote.
-
Mamluki wengine wawili wa Mossad watiwa nguvuni kaskazini mashariki mwa Iran
Jul 22, 2025 04:31Askari usalama wa Iran wamewatia nguvuni magaidi wawili wa Shirika la Ujasusi la Israel (MOSSAD) katika mkoa wa kaskazini mashariki wa Khorasan ya Kaskazini, unaopatikana kaskazini mashariki mwa nchi.
-
Iran: Hatutaachana na haki yetu ya kurutubisha urani
Jul 22, 2025 03:55Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu haina nia ya kuachana na mpango wake wa nyuklia, ikiwemo kurutubisha madini ya urani, licha ya uvamizi wa kijeshi wa mwezi uliopita wa Marekani na mutifaki wake wa kieneo, Israel.
-
Araqchi: Ufaransa, Ujerumani na Uingereza hazina mamlaka ya kuhuisha "Snapback Mechanism"
Jul 21, 2025 13:44Iran imesema kuwa Ufaransa, Ujerumani na Uingereza hazina hadhi ya kisheria, kisiasa wala ya kimaadili ya kuhuisha utekelezaji wa kile kinachojulikana kama Snapback Mechanism ya makubaliano ya nyuklia ya mwaka 2015. Snapback Mechanism ni utaratibu wa kurejesha vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Iran.