-
Araqchi: Kushiriki Uingereza katika mashambulizi dhidi ya Iran kutasajiliwa katika historia ya uhusiano wa nchi mbili
Mar 20, 2026 11:40Sayyid Abbas Araqchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amezungumza kwa simu na mwenzake wa Uingereza, Yvette Cooper, kuhusu taathira za vita vya kulazimishwa vya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Iran na hali ya mambo ya sasa katika eneo la Magharibi mwa Asia.
-
Baqaei: Raia wote wa US wanapaswa kutangaza kuchukizwa na vita haramu vya Trump
Mar 19, 2026 10:59Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa vita vya sasa si vita vya wananchi wa Marekani. Ismail Baqaei ameeleza haya katika ujumbe aliotuma katika mtandao wa kijamii wa X baada ya kujiuzulu Mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kupambana na Ugaidi wa Marekani, Joseph Kent.
-
Pezeshkian: Taathira za mashambulizi dhidi ya miundo mbinu ya nishati ya Iran zitaitatiza dunia nzima
Mar 19, 2026 10:50Rais Masoud Pezeshkian wa Iran ametuma ujumbe na kuandika kuwa: Mashambulizi dhidi ya miundo msingi ya nishati ya Iran yana taathira ambazo ukubwa wake utaitatiza dunia nzima.
-
Iran yatuma barua UN; yalalamikia mashambulizi ya US dhidi yake kutokea katika nchi za eneo
Mar 18, 2026 09:21Iran imetuma barua saba tofauti kwa Umoja wa Mataifa na Baraza la Usalama la umoja huo kuhusiana na mashambulizi ya Marekani dhidi yake kutokea katika nchi za kanda hii.
-
"Israel inadanganya, Iran haitutishii": Afisa wa ujasusi aliyeteuliwa na Trump ajiuzulu kwa sababu ya vita na Iran
Mar 18, 2026 08:27Mkuu wa Kituo cha Kitaifa cha Kupambana na Ugaidi nchini Marekani amejiuzulu baada ya kufichua yanayojiri nyuma ya pazia kuhusu vita vya nchi hiyo na Israel dhidi ya Iran.
-
Araqchi amwambia Guterres: Simamisheni uchokozi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran
Mar 17, 2026 12:13Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema: "Matatizo ya usafirishaji wa meli katika Mlango-Bahari wa Hormuz ni matokeo ya vita vilivyoanzishwa na Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel, na kila nchi au shirika la kimataifa linalojali amani na usalama lazima lilaani uhalifu wa tawala hizo mbili na kutoa wito wa kukomeshwa uchokozi wao wa kijeshi dhidi ya taifa la Iran."
-
Araqchi: Vita vitaisha kwa njia itakayomfanya adui asifikirie tena kutushambulia
Mar 17, 2026 10:31Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu haijatuma ujumbe wa aina yoyote kwa wavamizi wala haijaomba kusitishwa vita.
-
Pezeshkian: Iran haitasalimu amri mbele ya madola ya kibeberu
Mar 17, 2026 09:34Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesema taifa hili halitasalimu amri kamwe mbele ya madola ya kibeberu, huku akiitaka jamii ya kimataifa kulaani uvamizi wa Marekani na utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
IRGC: Tumewavurumishia maadui makombora 700, droni 3,600 mpaka sasa
Mar 17, 2026 07:08Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) limesema limepiga shabaha za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa makombora zaidi ya 700 na ndege zisizo na rubani 3,600 tangu Jamhuri ya Kiislamu ianzishe operesheni za kulipiza kisasi cha mashambulizi ya kichokozi ya maadui hao mwishoni mwa Februari mwaka huu.
-
Kamanda Naeini: Iran inadhibiti kikamilifu Lango Bahari la Hormuz
Mar 16, 2026 14:01Msemaji wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: Lango Bahari la Hormuz linadhibitiwa kikamilifu na Iran na kwamba uchokokozi wowote utakabiliwa na jibu kali.