-
Silaha za mauaji ya halaiki na sera za undumilakuwili za Washington na Tel Aviv, chanzo cha migogoro ya kiusalama Magharibi ya Asia
Nov 28, 2025 06:23Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Sayyid Abbas Araghchi amesema, yanayoendelea kujiri katika eneo la Magharibi ya Asia ambayo ni vita vya kudumu, uchokozi wa kivamizi, mauaji ya kimbari na kujipanua kikoloni utawala wa kizayuni wa Israel, ni matokeo ya moja kwa moja ya uungaji mkono wa Marekani na uridhishaji unaofanywa na baadhi ya nchi za Ulaya kwa utawala huo haramu.
-
Jeshi la Wanamaji la Iran kuzindia zana mpya za kivita
Nov 28, 2025 02:46Admeri Shahram Irani, Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Iran, ametangaza mipango ya kuzindua vifaa vipya na kuunganisha meli mpya katika jeshi hilo.
-
Haaretz: Netanyahu amepelekea Israel kushindwa katika pande zote, hususan dhidi ya Iran
Nov 26, 2025 12:18"Sera za waziri mkuu Benjamin Netanyahu zimepelekea kushindwa Israel katika pande zote za kidiplomasia, kijeshi, na kimkakati, hususan dhidi ya Iran". Hayo ni kwa mujibu wa Haaretz, gazeti la Israel linalochapishwa kwa lugha ya Kiebrania.
-
Asilimia 86 ya vijiji vya Iran vimeunganishwa kwa barabara za lami
Nov 26, 2025 07:14Wizara ya Uchukuzi ya Iran imesema kuwa karibu vijiji tisa kati ya kumi hapa nchini vimeunganishwa kwa barabara za lami; hatua inayoashiria upanuzi mkubwa wa miundombinu ya vijijini nchini Iran.
-
Marekani na nchi tatu za Ulaya zimeuaje Mkataba wa Cairo?
Nov 23, 2025 02:30Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameandika kwenye akaunti yake ya X kwamba: ""Mkataba wa Cairo" umeangamizwa na Marekani na nchi tatu za Ulaya."
-
Harakati ya pamoja ya kupinga hatua ya Magharibi dhidi ya Iran katika Bodi ya Magavana ya IAEA
Nov 22, 2025 10:20Hivi sasa kumejitokeza harakati ya pamoja ya kupinga hatua ya Troika ya Ulaya na Marekani dhidi ya Iran katika Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA).
-
Azimio jipya la Bodi ya Magavana ya IAEA lina lengo la kufidia kushindwa Marekani na Troika ya Ulaya
Nov 21, 2025 03:03Mwakilishi wa kudumu na balozi wa Iran katika taasisi za kimataifa zenye makao yake mjini Vienna Austria amesema kupitishwa azimio la kisiasa dhidi ya nishati ya nyuklia ya Iran yenye malengo ya amani ni jaribio la Marekani na Umoja wa Ulaya ili kufidia kushindwa kwao katika utaratibu wa Snapback huko New York.
-
Iran: Azimio la Marekani lililopasishwa na UN kuhusu Gaza linahalalisha ukaliaji mabavu
Nov 19, 2025 12:46Iran imekosoa azimio lililoandaliwa na Marekani na kupasishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linaloweka utaratibu wa kutumwa Gaza usimamizi wa nchi ajinabi na kutahadharisha kuwa azimio hilo linadhoofisha haki za msingi za watu wa Palestina.
-
Grossi: Wakaguzi wa wakala wa IAEA wamerejea Iran
Nov 19, 2025 12:05Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) amesema katika kikao cha robo mwaka cha Bodi ya Magavana ya wakala huo kwamba: "Wakaguzi wa IAEA wamerejea Iran na wamefanya ukaguzi katika vituo ambavyo havikuathiriwa na mashambulizi ya Juni, lakini ushirikishwaji zaidi unahitajika ili kurejesha ukaguzi kamili."
-
Rais Pezeshkian: Iran inalenga kuimarisha uhusiano na Oman
Nov 19, 2025 06:59Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesifu uhusiano imara kati ya Iran na Oman, na kueleza kuwa Tehran ina imani kwamba uhusiano wa pande mbili utaendelea kukua kwa "nguvu na uthabiti.