-
Raisi: Iran kamwe haitaruhusu kutengwa wanawake katika jamii
May 08, 2024 23:03Rais wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu katu haitakubali sera ambazo zitapelekea kutengwa wanawake katika jamii.
-
Eslami: Mienendo ya kiuhasama ya Israel isiathiri uhusiano wa Iran na IAEA
May 07, 2024 22:53Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) amesema hatua na mienendo ya kiuadui ya utawala wa Kizayuni wa Israel haipasi kuathiri uhusiano na ushirikiano baina ya Tehran na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA).
-
Safari ya Grossi nchini Iran na kuwekwa wazi maendeleo ya amani ya nishati ya nyuklia ya Iran
May 07, 2024 04:47Rafael Grossi, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA aliwasili mjini Tehran Jumatatu akiongoza ujumbe alioandamana nao kwa ajili ya kushiriki katika mkutano wa kimataifa wa nyuklia na vilevile kufanya mazungumzo na viongozi wakuu wa nyuklia na kisiasa wa nchini.
-
Iran ni ya nne duniani kwa uzalishaji wa elimu katika uwanja wa mimea ya dawa
May 06, 2024 22:49Katibu wa Kamati ya Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia ya Mimea ya Dawa na Tiba Asilia katika Ofisi ya Rais wa Iran ametangaza kuwa, watafiti wa Iran wanashika nafasi ya nne duniani katika uzalishaji wa sayansi katika uga wa uzalishaji wa mimea ya dawa na tiba asilia.
-
Rais wa Iran: Matukio ya Gaza yamefichua sura halisi ya Magharibi
May 06, 2024 07:13Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, matukio ya Gaza yamefichua sura halisi ya Wamagharibi na kuonyesha mgongano uliopo kati ya kambi ya watu sharifu, na tabaka la wanafunzi wenye uelewa wa vyuo vikuu na mrengo wa uovu wa viongozi wakorofi na wanaokanyaga sheria, haki na uhuru wa binadamu wa nchi za Magharibi.
-
Iran yapongeza uamuzi wa Uturuki kukata uhusiano wa kibiashara na utawala wa Israel
May 05, 2024 08:31Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amepongeza uamuzi wa serikali ya Uturuki wa kukata uhusiano wa kiuchumi na kibiashara na utawala wa Kizayuni wa Israel unaotekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza.
-
Abdollahian: Utawala wa Kizayuni wa Israel kamwe hauwezi kuwa halali kwa kupita zama
May 05, 2024 00:47Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Utawala wa Israel si serikali halali na utawala huo wa kibaguzi unaoukalia kwa mabavu Palestina kamwe hauwezi kuwa halali kwa kupita zama.
-
Sisitizo la Iran kuhusu Palestina kupewa uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa
May 04, 2024 23:37Amir Saeid Iravani, Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesisitiza umuhimu wa Palestina kuwa mwanachama kamili wa Umoja wa Mataifa.
-
Iran yalaani ukandamizaji unaofanywa na Serikali ya Marekani dhidi ya wanafunzi wanaoitetea Palestina
May 03, 2024 23:43Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Nasser Kan'ani amelaani hatua ya vyombo vya dola vya Marekani ya kukandamiza kwa mkono wa chuma maandamano ya wanafunzi wanaoitetea na kuiunga mkono Palestina yanayofanyika kwenye maeneo ya vyuo vikuu vya nchi hiyo.
-
Waziri wa Biashara na Viwanda wa Niger asisitiza juu ya kuimarisha uhusiano na Iran
May 03, 2024 07:13Waziri wa Biashara na Viwanda wa Jamhuri ya Niger amesisitiza kuhusu kuimarishwa uhusiano baina ya nchi yake na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika nyanja mbalimbali zikiwemo za kiuchumi.