-
Iran yalaani veto ya Marekani dhidi ya uanachama kamili wa Palestina UN
Apr 20, 2024 03:13Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani kura ya turufu ya Marekani dhidi ya rasimu ya azimio iliyotaka Palestina ipewe uanachama kamili katika Umoja wa Mataifa.
-
Vyombo vya habari: Iran imetungua ndege tatu zisizo na rubani katika mji wa Esfahan
Apr 19, 2024 04:28Vyombo vya habari vimeripoti kuwa, mfumo wa ulinzi wa anga wa Iran umetungua ndege tatu ndogo zisizo na rubani katika mkoa wa Esfahan ulioko katikati mwa nchi saa kadha baada ya vyombo vya habari vya Marekani kuwanukuu maafisa waandamizi wa nchi hiyo wakidai kwamba makombora ya utawala wa Kizayuni wa Israel yamepiga eneo la Iran.
-
SEPAH: Vitisho vya Israel dhidi ya Iran si vipya na Tehran muda wote iko tayari kujibu mashambulizi ya adui
Apr 18, 2024 10:00Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya nchini Iran SEPAH amesema kuwa, vitisho vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Iran haviwezi kuifanya Jamhuri ya Kiislamu kubadilisha sera na siasa zake kuhusu kustafidi kwa njia ya amani na teknolojia ya nyuklia.
-
Kukiri Pentagon kuhusu uwezo wa kijeshi wa Iran katika kuujibu utawala wa Kizayuni
Apr 18, 2024 08:49Patrick Ryder Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) amekiri juu ya nguvu za kijeshi za Iran katika kutoa jibu la kijeshi kwa utawala wa Israel.
-
Iran: Marekani ilikuwa na taarifa kuhusu Operesheni ya Ahadi ya Kweli ya kuutia adabu utawala wa Israel
Apr 18, 2024 04:01Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, Jamhuri ya Kiislamu iliikuwa imeshaitaarifu serikali ya Marekani kabla ya kutekeleza Operesheni ya Ahadi ya Kweli ya kuutia adabu utawala wa Israel mfanyamauaji ya kimbari.
-
Borrell: Ukraine isiombe kupewa msaada na Magharibi kama iliopewa Israel katika shambulio la Iran
Apr 18, 2024 02:19Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya Josep Borrell amesema, Ukraine haipaswi kuomba msaada wa aina ile ile ambayo nchi za Magharibi zilitoa kwa Israel wakati wa shambulio la kijeshi la Iran kwa sababu hali hizo mbili haziwezi kulinganishwa.
-
Iran iliwasiliana na nchi za eneo katika kutekeleza Operesheni ya Ahadi ya Kweli dhidi ya Israel
Apr 17, 2024 07:19Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran anayehusika na masuala ya kisiasa amesema: Iran ilikuwa ikiwasiliana na nchi za eneo katika mchakato wa kutoa jibu kwa utawala wa Kizayuni na utekelezaji wa Operesheni ya Ahadi ya Kweli.
-
Grossi asisitiza tena kutokuwepo shughuli za kijeshi za nyuklia nchini Iran
Apr 16, 2024 22:58Rafael Grossi, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA amesisitiza kuwa, hakuna nyaraka zozote zinazothibitisha utengenezaji wa silaha za nyuklia nchini Iran na kuwa, mivutano ya hivi sasa haijavuruga mchakato wa ufuatiliaji wa wakala huo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran.
-
Amir-Abdollahian: Iran haitoruhusu Israel kuhatarisha usalama wa ukanda huu
Apr 16, 2024 07:19Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaamini kwamba usalama na utulivu wa nchi za eneo hili zima ni muhimu sana kwake, bali ni sawa kabisa na usalama wake yenyewe na haitoruhusu utawala wa Kizayuni kuhatarisha usalama wa eneo hili kwa chokochoko zake.
-
Kikao cha Baraza la Usalama: Uwanja wa makabiliano kati ya waungaji mkono wa Iran na Wamagharibi wanaounga mkono utawala wa Kizayuni.
Apr 16, 2024 04:24Kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kujadili mashambulizi ya Iran ya kuuadhibu utawala wa Israel kilifanyika Jumapili jioni tarehe 14 Aprili, kikao ambacho kilibadilika na kuwa uwanja wa makabiliano kati ya nchi zinazounga mkono Iran na kambi ya Magharibi waitifaki wa utawala wa Kizayuni.