-
Iran yashinda viti 2 vya kimataifa katika Shirika la Hali ya Hewa Duniani
Jul 07, 2024 01:10Bahareh Arabi, Mkuu wa Idara ya Kimataifa ya Shirika la Hali ya Hewa la Iran amesema wataalamu 2 wa Shirika la Hali ya Hewa la Iran wamechaguliwa kuwa wajumbe wa Tume ya Huduma ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani.
-
Sisitizo la kupanuliwa uhusiano wa Iran na China
Jul 06, 2024 22:54Mohammad Mokhbrr, Kaimu Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Rais Xi Jinping wa China walikutana na kujadiliana kando ya Mkutano wa 24 wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai huko Astana, mji mkuu wa Kazakhstan.
-
Muda wa kupiga kura kwenye uchaguzi wa rais Iran warefushwa
Jul 05, 2024 11:25Muda wa kupiga kura katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais wa Iran iliyoanza mapema leo kote nchini, umerefushwa kwa saa mbili, hiyo ikiwa na maana kuwa zoezi hili litaendelea hadi saa mbili usiku kwa saa za hapa nchini.
-
Duru ya pili ya uchaguzi wa Rais wa Iran yaakisiwa kwa wingi duniani
Jul 05, 2024 07:43Vyombo vya habari vya duniani vimeakisi kwa wingi mno duru ya pili ya uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Kisilamu ya Iran kutokana na watu kujitokeza kwa mamilioni katika uchaguzi huo wa leo Ijumaa.
-
Mokhber: Uhusiano wa kimkakati wa Iran, Russia umebadilisha milingano ya dunia
Jul 04, 2024 23:26Kaimu Rais wa Iran amesema uhusiano wa kistratajia baina ya Jamhuri ya Kiislamu na Russia umebadilisha mlingano wa nguvu duniani, na kukabiliana na mfumo usio wa kiadilifu na unaoegemea upande mmoja wa Marekani.
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu juu ya umuhimu wa kushiriki wananchi katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais
Jul 04, 2024 08:01Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameeleza umuhimu wa kushiriki kwa wingi wananchi katika duru ya pili ya uchaguzi wa Rais wa Iran na kusisitiza kuwa, kadiri ushiriki wa wananchi unavyokuwa mkubwa ndivyo serikali pia itakavyoweza kutimiza malengo yake ndani ya nchi na kufuatilia malengo mbalimbali katika kalibu ya mkakati mkuu wa nchi.
-
Vikwazo, dhulma na jinai: Mhimili wa haki za binadamu wa Marekani dhidi ya taifa la Iran
Jul 03, 2024 04:32Ali Bagheri Kani, Kaimu Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesema ukiukaji wa haki za watu wa Iran vikiwemo vikwazo vya kidhalimu dhidi yao, ndio msingi wa haki za binadamu wa Marekani.
-
Mwanadiplomasia wa Iran atahadharisha kuhusu taathira za vita vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Lebanon
Jul 02, 2024 08:23Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ambaye pia ni Mkuu wa Baraza la Kistratejia la Uhusiano wa Nje la Iran ametahadharisha kuhusu mashambulizi yanayoweza kuanzishwa na utawala unaotekeleza mauaji ya kimbari wa Israel dhidi ya Lebanon.
-
Kamanda Hajizadeh: Muqawama wa Palestina lazima utapata ushindi Gaza
Jul 02, 2024 03:38Kamanda wa Kikosi cha Anga za Mbali cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema hakuna chembe ya shaka kuwa muqawama wa Palestina utapata ushindi wa 'kishindo' mkabala wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Bagheri: Waliomuunga mkono Saddam katika jinai ya Sardasht wanaunga mkono jinai za Wazayuni Ukanda wa Gaza
Jul 02, 2024 00:43Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika siku ya kumbukumbu ya mashambulizi ya silaha za kemikali katika mji wa Sardasht nchini Iran kwamba: Wale waliounga mkono jinai za utawala wa Saddam Hussein dhidi ya watu wa Sardasht nchini Iran hivi sasa wanaunga mkono jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel huko Ukanda wa Gaza.