-
Onyo la Iran kwa Marekani na Magharibi kuhusu madhara yatakayozipata zikiiunga mkono Israel
Apr 15, 2024 08:32Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeionya na kuitahadharisha Marekani na nchi za Magharibi juu ya kuuunga mkono kijeshi utawala wa Kizayuni na kufanya chokochoko dhidi ya Iran na kutangaza kwamba, iwapo nchi hizo zitaingilia kati katika kuuunga mkono utawala wa Kizayuni, vituo vyao vyote na maeneo yote ya maslahi yao yatashambuliwa na vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Iran haitasita kulinda maslahi yake
Apr 15, 2024 01:00Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitasita wala kuwa na shaka katika kulinda maslahi yake halali dhidi ya uchokozi wowote mpya.
-
Rais Raisi: Hatua yoyote ya kifidhuli itakabiliwa na jibu kali zaidi la Iran
Apr 14, 2024 07:42Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utafanya harakati yoyote ya kifidhuli utakabiliwa na jibu madhubuti, zito na kali zaidi.
-
Balozi wa Iran UN: Jibu la Iran litakuwa kali zaidi iwapo Israel itaanzisha tena mashambulizi
Apr 14, 2024 04:15Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa ametangaza katika barua kwa Baraza la Usalama kwamba ikiwa utawala wa Israel utaanzisha tena mashambulizi yoyote ya kijeshi, bila shaka jibu la Iran litakuwa la nguvu na kali zaidi.
-
Khalid Mash'al: Karibuni hivi, vita vya miezi sita vitamvunja adui Mzayuni
Apr 13, 2024 23:01Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya ughaibuni ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS Khaled Mash'al, amepongeza istiqama ya kishujaa ya Ukanda wa Ghaza na kusisitiza kuwa vita vya miezi sita wanavyopigana Wapalestina na utawala wa Kizayuni wa Israel "karibuni hivi vitamvunja adui Mzayuni".
-
Ombi la Rais wa Marekani kwa Iran: Msiishambulie Israel
Apr 13, 2024 08:39Rais wa Marekani kwa mara nyingine tena, katika uingiliaji wa wazi na kuunga mkono utawala wa Israel, ameiomba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran isijibu mashambulizi ya utawala huo kwenye ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus huko Syria.
-
Raisi: Madola ya kibeberu yanazusha fitna ili kuvuruga usalama kati ya Iran na Pakistan
Apr 12, 2024 07:48Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, kustawishwa uhusiano wa Iran na Pakistan hakufurahishi madola ya kibeberu na kwa hivyo yanazusha fitna ili kuleta mpasuko kati ya mataifa hayo mawili na nchi hizo mbili za Kiislamu.
-
Mwakilishi wa Iran UN asisitiza ulazima wa kuuadhibu utawala vamizi wa Israel
Apr 12, 2024 04:10Ofisi ya Mwakilishi wa Iran katika Umoja wa Mataifa imesema Baraza la Usalama lilipaswa kulaani mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya maeneo ya kidiplomasia ya Iran huko Damascus, mji mkuu wa Syria.
-
Amir Abdollahian: Kujilinda kwa lengo la kumuadhibu mchokozi ni jambo la lazima
Apr 11, 2024 23:57Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Jamhuri ya Kislamu ya Iran amesema kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel unapokiuka kikamilifu kinga ya watu binafsi na maeneo ya kidiplomasia kwa kukanyaga sheria za kimataifa na Mikataba ya Vienna, inakuwa lazima kujihami kwa lengo la kumuadhibu mchokozi.
-
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Imarati, Uturuki wajadiliana matukio ya Ghaza
Apr 11, 2024 06:24Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza katika mazungumzo yake ya simu na mawaziri wenzake wa Muungano wa Falme za Kiarabu (Imarati) na Uturuki kwamba kuna udharura wa kukomeshwa haraka jinai za utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza.