-
Pezeshkian amweleza Erdogan: Iran inapinga vitisho, inaunga mkono mazungumzo na diplomasia
Jan 30, 2026 23:27Iran inapinga vitisho na kushurutishwa na ina azma thabiti ya kufanya mazungumzo, kuheshimiana pande mbili na kutekelezwa diplomasia kwa manufaa ya pande zote. Haya yameelezwa na Rais Masoud Pezeshkian huku Washington ikiendelea kutoa vitisho vya kijeshi dhidi ya Tehran.
-
Araqchi: Iran iko tayari kwa vita na mazungumzo
Jan 30, 2026 23:16Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, amesema kuwa Tehran iko tayari kwa vita na mazungumzo lakini haitakubali kuwekewa masharti. Araqchi ameeleza haya kufuatia vitisho vya kijeshi vya Washington dhidi ya Tehran.
-
Kucheza na moto kwa Trump kunaweza kusababisha mzozo kamili kanda ya Asia Magharibi
Jan 30, 2026 08:30Iran imetangaza kwamba kauli za "kuchochea vita" za Donald Trump zinazidisha mvutano wa kikanda.
-
'Hakuna vita vya masaa 2', yasema Iran ikiapa kutoa jibu la haraka kwa uchokozi wa US au Israel
Jan 30, 2026 04:17Jeshi la Iran limetoa onyo kali kwamba kitendo chochote kipya cha uchokozi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu kitakabiliwa na jibu kali na la haraka, likisisitiza kwamba uzoefu na tajiriba ya vita vya Juni vimebadilisha kimsingi muelekeo wa kijeshi wa Iran na kanuni zake za makabiliano.
-
Afisa mwandamizi wa jeshi la Israel: Iran ni dola moja kuu kwa makombora duniani
Jan 30, 2026 04:17Kamanda wa zamani wa mitambo ya ulinzi wa anga wa utawala wa kizayuni wa Israel ameielezea Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuwa ni moja ya madola makuu duniani kwa upande wa masuala ya anga na ulimwengu wa makombora, na akasema, Tehran itailenga Tel Aviv iwapo kutakuwa na shambulio lolote litakalofanywa na Marekani dhidi yake.
-
Qalibaf: Iran haipingi mazungumzo, inataka diplomasia ichukue mkondo wake
Jan 29, 2026 23:42Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesema kuwa Tehran haipingi msingi wa mazungumzo na diplomasia ambao lazima uwe wa aina yake na wenye mlingano kwa mujibu wa kuheshimiana pande mbili.
-
'Ni rahisi - Trump ameshindwa': Wanamtandao wakosoa vitisho vya kijeshi vya Marekani dhidi ya Iran
Jan 29, 2026 09:35Watumiaji wa mitandao ya kijamii wamekosoa vitisho vya kijeshi vya mara kwa mara vya Rais wa Marekani, Donald Trump dhidi ya Iran, ambapo hivi karibuni alitishia Iran kwa kisingizio cha miradi ya nyuklia ya nchi hiyo. Wamesema kuwa Israel inaiburuta Washington katika vita vingine kwa niaba ya serikali ya Tel Aviv.
-
Nujaba kwa maadui wa Iran: Vita vinaweza kufika milangoni kwenu
Jan 29, 2026 02:57Katibu Mkuu wa kundi la kupambana na ugaidi la Harakat al-Nujaba la Iraq amewaonya vikali maadui wa Iran kuhusu matokeo mabaya ya uchokozi wowote mpya ambao wanaweza kufanya dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Araghchi: Mazungumzo hayawezi kufanikiwa chini ya vitisho
Jan 29, 2026 00:19Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi ameonya kwamba, kutwisha diplomasia kupitia vitisho vya kijeshi hakuwezi kuwa na ufanisi au tija, akisema kwamba hakuna uamuzi wowote ambao umefanywa na Tehran kufikia juu ya kufanya mazungumzo na Marekani.
-
Iran: Maadui wajiandae kwa 'jibu la uharibifu' wakituchokoza
Jan 29, 2026 00:18Kamanda mwandamizi wa Jeshi la Iran ameonya kwamba, hatua yoyote ghalati dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu itawasababishia maadui uharibifu mkubwa, akisisitiza kwamba vitisho dhidi ya Tehran kupitia maonyesho ya kijeshi havilishughulisha taifa hili.