-
Iran, China na Russia zailaani Marekani kwa ghasia za karibuni nchini Iran
Jan 16, 2026 03:49Gholamhossein Darzi, Naibu Mwaklishi wa Kudumu wa Iran Umoja wa Mataifa ameikosoa vikali Marekani katika mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu ghasia na machafuko yaliyoungwa mkono na nchi ajinabi dhidi ya Iran.
-
Jumuiya ya Shanghai yalaani ghasia za kigaidi nchini Iran huku uungaji mkono kimataifa ukiongezeka
Jan 16, 2026 03:48Norlan Yerkembayev Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai (SCO) amelaani vikali hujuma za kigaidi na uharibifu wa hivi karibuni katika mji wa Tehran na miji mingine ya Iran iliyoathiriwa wakati wa maandamano ya amani ya wananchi.
-
Iran: US, Israel ziliwapa silaha, fedha wafanya ghasia nchini
Jan 15, 2026 23:24Waziri wa Ulinzi wa Iran amesema Marekani na Israel zilipanga na kufanikisha ghasia zilizoshuhudiwa hapa nchini hivi karibuni, zikielekeza silaha na pesa taslimu kuchochea vurugu na uvunjifu wa utulivu, ikiwa ni sehemu ya mpango mpana wa kuibua mgawanyiko na mifarakano katika taifa hili.
-
ANC yaonya kuhusu njama za 'mapinduzi' nchini Iran
Jan 15, 2026 22:43Mkuu wa vuguvugu la Mshikamano wa Kimataifa wa chama tawala cha African National Congress (ANC) katika jimbo la Western Cape nchini Afrika Kusini ameonya kwamba, machafuko ya hivi karibuni nchini Iran yana mkono wa Marekani na washirika wake wa Kizayuni.
-
Nini lengo la mchezo wa takwimu wa Trump kuhusu waliofariki katika ghasia za Iran?
Jan 15, 2026 07:04Ikiwa ni katika fremu ya uingiliaji wake katika masuala ya ndani ya Iran, Rais Donald Trump wa Marekani amezindua sarakasi mpya ya takwimu kuhusu Iran.
-
Araghchi amwandikia barua Katibu Mkuu wa UN kuhusiana na machafuko na jinai zilizofanywa na magaidi mamluki nchini Iran
Jan 15, 2026 06:58Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemwandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusiana na jinai zilizofanywa na magaidi mamluki katika machafuko na uvurugaji wa amani uliofanywa hivi karibuni hapa nchini.
-
Russia: Badala ya Ulaya kuzungumzia hali ya Iran ifuatilie kuiokoa Greenland
Jan 15, 2026 06:57Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia, Maria Zakharova amesema, badala ya viongozi wa Umoja wa Ulaya, EU kutoa matamshi ya kuzungumzia hali ya Iran, ingekuwa bora kama wanegejikita kushughulikia kadhia ya Greenland, ambayo sasa hivi Marekani inafanya juu chini kuitia mkononi.
-
Kwa nini Pakistan imekosoa msimamo wa Trump kuhusu machafuko nchini Iran?
Jan 14, 2026 03:51Pakistan imekosoa msimamo wa Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu machafuko yanayochochewa na nchi za Magharibi nchini Iran.
-
Larijani: Trump ndiye 'muuaji mkubwa zaidi' wa Wairani
Jan 14, 2026 03:16Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC) amelaani vitisho vya Rais wa Marekani Donald Trump dhidi ya taifa hili, akimtaja mwanasiasa huyo kama mmoja wa wauaji wakubwa zaidi wa Wairani.
-
Araghchi atoa onyo baada ya vitisho vya Trump: Iran iko tayari kwa vita ikiwa Marekani inataka 'kuvijaribu'
Jan 13, 2026 07:01Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi ameionya Marekani kwamba, Tehran "iko tayari kwa machaguo yote" baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kutishia kuchukua hatua za kijeshi sambamba na Iran kukabiliwa na machafuko hivi karibuni yaliyochochewa na kuungwa mkono na maadui wa nje ya nchi.