-
Jitihada za kufunga kituo cha Kiislamu cha Hamburg, Ujerumani
Nov 12, 2022 08:48Katika juhudi za madola ya Magharibi za kuunga mkono ghasia na machafuko nchini Iran, vyama vya muungano unaotawala nchini Ujerumani vimetoa wito wa kufungwa Kituo cha Kiislamu na Kiutamduni cha Iran katika mji wa Hamburg nchini humo.
-
Amir Abdollahian: Azimio la UN haliizuia Iran kuuza silaha nje ya nchi
Nov 12, 2022 04:40Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesema: "Kwa mujibu wa azimio nambari 2231 la Baraza la Usalama, hakuna marufuku ya kuagiza na kuuza silaha za Iran nje ya nchi, na Tehran haijaipa Russia silaha zozote ili zitumike katika vita vya Ukraine."
-
Faili la pili la sauti ya mwandishi wa BBC: Lengo la ghasia ni kuigawa Iran
Nov 11, 2022 04:37Faili la pili la sauti lililovuja la mwandishi wa Shirika la Utangazaji la Uingereza BBC limefichua wazi zaidi jinsi televisheni inayofadhiliwa na Saudia inayojiita 'Iran International' inavyoongoza kampeni ya kuigawa Iran vipande vipande.
-
Iran yaionya Ujerumani: Jibu letu kwa uingiliaji wenu litakuwa zito
Nov 10, 2022 07:37Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekosoa vikali matamshi ya uingiliaji na ya kichochezi yaliyotolewa na mwenzake wa Ujerumani na kuonya kuwa, Tehran itatoa jibu lenye mlingano na madhubuti kwa misimamo hiyo ya uingiliaji wa masuala ya ndani ya nchi hii.
-
Sisitizo jingine la Marekani la kuunga mkono vurugu na machafuko nchini Iran
Nov 09, 2022 05:12Ned Price, msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani ameendelea kuunga mkono vurugu na machafuko nchini Iran na kukana kabisa kuhusika nchi yake katika vurugu hizo.
-
Mkuu wa sera za nje wa EU atoa madai mapya kuhusu mazungumzo ya Vienna
Nov 08, 2022 04:37Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya ametoa madai mapya kuhusu mazungumzo ya Vienna ya uondoaji vikwazo dhidi ya Iran pasina kuashiria chochote kuhusu kujiondoa kinyume cha sheria Marekani katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA na jinsi nchi za Ulaya zilivyohalifu ahadi zao kuhusiana na makubaliano hayo.
-
Rais wa Ufaransa: Inapasa tubadilishe mbinu ya kukabiliana na Iran
Nov 08, 2022 03:59Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa amedai kuwa vitisho vya Iran vimevuka mipaka ya Asia Magharibi, na kueleza kwamba mbinu za kukabiliana na vitisho vya Tehran duniani inapasa zibadilishwe.
-
Iran na Zimbabwe zatathmini njia za kuimarisha uhusiano wao
Nov 06, 2022 04:18Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Zimbabwe hapa mjini Tehran, na kujadili mikakati na njia za kupanua na kuboresha uhusiano wa pande mbili wa nchi hizi mbili.
-
Jibu la Rais wa Iran kwa bwabwaja na njozi za Biden
Nov 05, 2022 07:57Rais Sayyid Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika marasimu ya kukumbuka tarehe 13 Aban ambayo inaadhimishwa hapa nchini kama Siku ya Kitaifa ya Kupambana na Uistikbari Duniani kwamba: Marekani ina nafasi ya kwanza katika vita na umwagaji damu na inaangamiza na kuharibu maslahi ya mataifa mengine ili kujidhaminia maslahi yake. Rais wa Iran ameeleza hayo katika radiamali yake kwa matamshi ya Joe Biden ya kuuunga mkono ghasia na fujo nchini Iran.
-
Sheikh Kazem Sediqi: Lengo la Marekani ni kuchochea hisia za kikaumu nchini Iran
Nov 04, 2022 08:24Khatibu wa Swala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo hapa mjini Tehran amesema kuwa, lengo la utawala wa Marekani katika fitina na vurugu za hivi karibuni hapa Iran ni kuchochea hisia za kikaumu na kuzusha vita vya ndani katika taifa hili.