-
Onyo la Mkuu wa Kamandi ya Majeshi ya Iran kwa Israel
Jun 27, 2022 06:55Kamanda mkuu wa vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameuonya vikali utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya kuchukua hatua yoyote ya kichokozi katika eneo la Asia Magharibi na kusisitiza kuwa, sera ya Israel ya kuingilia mambo ya ndani ya nchi nyingine na chokochoko zozote za utawala huo katika eneo zitakabiliwa na jibu mwafaka.
-
Malengo ya safari ya Mustafa al Kadhimi mjini Tehran
Jun 27, 2022 06:09Mustafa la Kadhimi, Waziri Mkuu wa Iraq, baada ya kukutana na wakuu wa Saudi Arabia mjini Jeddah, moja kwa moja ameelekea Tehran Jumapili Juni 26 na kulakiwa rasmi na Rais Ebrahim Raeisi wa Iran.
-
Wazayuni wameingiwa na hofu kutokana na safari ya Mkuu wa Sera za Nje wa EU Tehran
Jun 27, 2022 03:36Waziri wa mambo ya nje wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel, ambaye kila mara amekuwa akifanya uafriti na kuweka pingamizi dhidi ya mpango wa kuiondolea Iran vikwazo vya kidhalimu, ametoa matamshi ya uropokaji ya kukosoa safari ya Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya hapa mjini Tehran.
-
Rais wa Iran afanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Iraq mjini Tehran
Jun 26, 2022 10:10Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mchana wa leo amemlaki rasmi Waziri Mkuu wa Iraq hapa Tehran.
-
Shamkhani: Iran inataka makubaliano thabiti na ya kudumu
Jun 26, 2022 06:49Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu ipo tayari kufikia makubaliano thabiti, ya kudumu na ya kutegemewa baina yake na kundi la 4+1 katika mazungumzo ya kujaribu kuhuisha mapatano ya nyuklia ya JCPOA huko Vienna, Austria.
-
Raisi: Iran haitaondoka kwenye meza ya mazungumzo ya JCPOA
Jun 26, 2022 03:47Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: Iran haitaondoka kwenye meza ya mazungumzo kwa ajili ya kuondolewa vikwazo.
-
Amir-Abdollahian: Iran inataka iwe na uhusiano na dunia ulio na uwiyano
Jun 25, 2022 08:11Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, Iran inataka iwe na uhusiano na dunia ulio na uwiyano na kudumisha sambamba na kupanua uhusiano wake na bara la Ulaya.
-
Raeisi: Iran ni mshirika endelevu wa BRICS katika nishati
Jun 24, 2022 23:51Rais Ebrahim Raeisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Iran inaweza kuwa mshirika endelevu wa kuunganisha nchi wanachama wa BRICS katika maeneo muhimu ya kupitisha nishati na masoko makubwa duniani kwa kuzingatia nafasi yake ya kipekee ya jiografia ya kisiasa na jiografia ya kiuchumi.
-
Iran: Mataifa ya Asia Magharibi yanapaswa kuamua kuhusu mustakabali wa eneo
Jun 24, 2022 07:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema mataifa ya Asia Magharibi ndiyo yanayostahiki kuamua kuhusu mustakabali wa eneo hili la kistratijia.
-
Khatibzadeh: Uturuki isiyanyamazie madai ya kufarakanisha ya Wazayuni
Jun 24, 2022 03:37Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Iran amesema, inatarajiwa kuwa Uturuki haitanyamazia kimya madai ya kufarakanisha yaliyotolewa na wazayuni.