-
Russia: Wapinzani wa JCPOA wanakusudia kudunisha ushirikiano wa Iran na IAEA
May 25, 2020 21:56Mwakilishi wa kudumu wa Russia katika mashirika ya kimataifa yenye makao yao mjini Vienna nchini Austria amesema wapinzani wa makubaliano ya nyuklia yaliyosainiwa baina ya Iran na madola makubwa duniani mwaka 2015 wanalenga kudunisha na kudhalilisha muamana na ushirikiano baina ya Tehran na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA).
-
Sisitizo la Venezeula kuhusu kutokuwa na maana vitisho vya Marekani dhidi ya meli za mafuta za Iran
May 25, 2020 06:01Wakati wa utawla wa rais Donald Trump wa Marekani, sera za mashinikizo ya pande zote dhidiya Venezeula zimeongezeka kwa kuwekewe vikwazo vingi nchi hiyo lengo likiwa ni kuipindua serikali ya Rais Nicolas Maduro na kumleta madarakani kinara wa wapinzani Juan Guaid ambaye ni kibaraka wa Washington.
-
Zarif: Natumai ulimwengu wa Kiislamu utapata ushindi dhidi ya maadui
May 24, 2020 06:23Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameeleza matumaini yake kuwa ulimwengu wa Kiislamu utaibuka na ushindi dhidi ya maadui.
-
Brig. Jen. Hajizadeh: Utayarifu wa kujihami Iran upo katika kiwango cha juu zaidi
May 24, 2020 06:16Kamanda wa Kikosi cha Anga za Mbali cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema kuwa, utayarifu wa kulihami na kulilinda wa taifa la Iran hivi sasa upo katika kiwango cha juu zaidi katika historia ya Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Uingereza yachukizwa na hotuba ya Kiongozi Muadhamu ya kuitetea Palestina
May 23, 2020 22:21Hotuba ya kistratijia na ya kutia matumaini ya Kiongozi Muadhamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei katika kuitetea Palestina na kufichua njama chafu za utawala haramu wa Kizayuni wa Israel na waungaji mkono wake, imewatia hasira viongozi wa Uingereza.
-
Wizara ya Ulinzi ya Iran: Tutaendelea kuunga mkono muqawama wa Palestina
May 23, 2020 05:45Wizara ya Ulinzi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema itaendelea kuziunga mkono na kuzipa misaada isiyo na kikomo harakati za muqawama za Palestina zinazopambana na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Iran; jitihada zisizo na tija za utawala wa Trump
May 23, 2020 02:45Baada ya kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya Iran mnamo Mei 2018, serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani imekuwa ikitekeleza mashinikizo ya juu kabisa kwa kuiwekea Iran vikwazo shadidi zaidi kuwahi kushuhudiwa katika historia. Pamoja na kuwa vikwazo hivyo havijaweza kufanikiwa, Marekani inasisitiza kuendelea na sera yake hiyo ya vikwazo.
-
Jihadul Islami: Iran inahimili vikwazo vya kila namna kwa ajili ya kuihami Palestina
May 22, 2020 22:06Mjumbe wa Ofisi ya Kisiasa ya harakati ya Jihadul Islami ya Palestina amegusia maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Quds yaliyofanyika jana Ijumaa kote duniani na kukumbusha kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imejikubalisha kuhimili na kuvumilia mashinikizo na vikwazo vya kila namna vya mabeberu kwa ajili ya kuhami malengo matukufu ya Palestina.
-
Russia na Venezuela zakosoa hatua zisizo za kisheria za Marekani
May 22, 2020 02:00Tangu Rais Donald Trump mwenye kashfa nyingi wa Marekani aingie ikulu ya White House ameshadidisha siasa za uhasama dhidi ya Venezuela ambapo pia amefanya njama nyingi za kuiondoa madarakani serikali halali ya Rais Nicolás Maduro wa nchi hiyo sambamba na kuiwekea vikwazo vikali.
-
Ijumaa, tarehe 22 Mei, 2020
May 21, 2020 22:09Leo ni Ijumaa tarehe 28 Ramadhan mwaka 1441 Hijiria, inayosadifiana na Pili Khordad 1399 Hijria Shamsia sawa tarehe 22 Mei mwaka 2020 Miladia.