-
Iran yalaani kitendo cha Israel cha kumtesa mwanaharakati Greta Thunberg
Oct 20, 2025 03:13Esmail Baqaei Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani vikali kitendo cha utawala wa Kizayuni wa Israel cha kumtesa mwanaharakti wa haki za binadamu aliyedhihirisha mshikamano na watu wa Palestina. Baqaei amevitaja vitendo hivyo vya Israel kuwa vya ukatili, visivyo vya kibinadamu na vya udhalilishaji.
-
Iran yailaani Israel kwa kuendelea kuua wanawake na watoto Gaza
Oct 19, 2025 03:10Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran, Esmaeil Baghaei amelaani ukiukaji wa mara kwa mara wa makubaliano ya usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza unaofanywa na utawala ghasibu wa Israel, likiwemo shambulio la hivi karibuni dhidi ya gari lililokuwa limebeba familia ya Kipalestina wakati ikirejea kwenye makazi yao.
-
China, Iran na Russia zathibitisha; Muda wa Azimio Nambari 2231 umemalizika
Oct 19, 2025 03:09Iran, China na Russia zimemwandikia barua ya pamoja Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, kuthibitisha kumalizika muda wa Azimio Nambari 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UNSC) kuhusu mpango wa amani wa nishati ya nyuklia wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Kumalizika muda wa Azimio 2231 la Baraza la Usalama; Iran yasisitiza kuondolewa vikwazo, yaungwa mkono na nchi 121
Oct 18, 2025 09:11Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa taarifa ikitangaza kumalizika muda wa Azimio nambari 2231.
-
Iran yakadhibisha madai kwamba inatishia usalama wa Uingereza
Oct 18, 2025 04:20Ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini London umepinga vikali madai ya mkuu wa Shirika la Ujasusi la Ndani la Uingereza (MI5) kwamba Tehran inataka kutishia usalama wa Uingereza, na kuyataja madai hayo kuwa "yasiyo na msingi."
-
Iran yalaani mashambulizi ya karibuni ya Israel kusini mwa Lebanon
Oct 18, 2025 04:19Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani mashambulizi ya karibuni ya anga ya Israel kusini mwa Lebanon, na kuzibebesha dhima nchi zilizodhamini makubaliano ya kusitisha vita yaani Ufaransa na Marekani kwa kutoichukulia hatua Israel.
-
Yazdanian: Iran hurusha satelaiti sita angani kila mwaka
Oct 18, 2025 04:18Vahid Yazdanian Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti wa Anga cha Iran ametangaza kuwa Iran imefanikiwa kurusha satelaiti sita angani kila mwaka, sambamba na kupiga hatua kubwa katika teknolojia ya kurusha satelaiti.
-
Unyanyuaji Uzani; Muirani avunja rekodi ya dunia, ashinda dhahabu Misri
Oct 17, 2025 03:20Ali Akbar Gharibshahi, bingwa wa mchezo wa kunyanyua vitu vizito wa Iran ameweka rekodi mpya ya dunia na kushinda medali ya dhahabu katika kategoria ya kilo wanamichezo wenye 107, kwenye Mashindano ya Dunia ya Kunyanyua Uzani ya 2025 nchini Misri.
-
Pezeshkian: Vijana wa Iran wamebobea katika uzalishaji wa makombora
Oct 16, 2025 23:12Rais Masoud Pezeshkian wa Iran ameashiria uwezo wa kustaajabisha wa vijana wa Jamhuri ya Kiislamu na kusisitiza kuwa, vijana wa taifa hili ndio ambao wanatengeneza makombora na nishati ya nyuklia kwa kutegemea uwezo wao.
-
Kharrazi: Iran iko tayari kwa mazungumzo, lakini haitakubali kuburuzwa
Oct 16, 2025 06:12Mkuu wa Baraza la Kistratijia la Mahusiano ya Kigeni ya Iran, Kamal Kharrazi amesema Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kwa mazungumzo, lakini katu haitakubali kutwishwa matakwa ya aina yoyote.