-
Qalibaf: Muda wa kumdhibiti mbwa kichaa wa Kizayuni unayoyoma
Aug 15, 2025 23:27Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa, Gaza ndiyo "ngome ya mwisho" ya Waislamu, na kusisitiza haja ya kuungwa mkono Palestina haraka iwezekanavyo, kabla ya ardhi nyingine katika eneo kushambuliwa na kuporwa na utawala ghasibu wa Israel.
-
MSF: Kipindupindu 'kibaya' kuwahi kutokea ndani ya miaka mingi kimeua watu 40 Darfur, Sudan
Aug 15, 2025 03:59Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) limeripoti kuwa, watu wasiopungua 40 wamefariki dunia katika eneo la Darfur, Sudan katika kipindi cha wiki moja, huku nchi hiyo ikikabiliana kudhibiti mripuko mkubwa zaidi wa kipindupindu kuwahi kushuhudiwa nchini humo katika kipindi cha miaka mingi.
-
Je, miradi ya pamoja ya mpakani kati ya Iran na Azerbaijan imeingia katika hatua mpya?
Aug 15, 2025 03:16Katika siku za hivi karibuni, sisitizo la viongozi wa Iran na Azerbaijan la kuharakisha miradi ya pamoja ya mpakani kwa mara nyingine tena limewavutia wachambuzi wa masuala ya kieneo kuhusu uhusiano wa nchi mbili hizi.
-
Iran: Haki ya kimsingi ya kujilinda iliyonayo Lebanon inaifanya ihitaji kuwa na uwezo wa kijeshi
Aug 11, 2025 07:52Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kwamba, kuwa na uwezo wa kijeshi ni muhimu kutokana na haki ya kimsingi ya kujilinda iliyonayo Lebanon.
-
Araqchi: Afisa wa IAEA Tehran, lakini hakuna mpango wa kukaguliwa maeneo ya nyuklia
Aug 11, 2025 05:37Abbas Araqchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) anatarajiwa kufanya ziara hapa Tehran kwa mazungumzo, lakini kutembelea taasisi za nyuklia si sehemu ya ajenda ya safari hiyo.
-
Iran yazindua kliniki 9 kote nchini za kutibu majeraha kwa kutumia plasma
Aug 11, 2025 05:35Mohammad Eslami, Makamu wa Rais na Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) ametangaza kuzinduliwa kliniki tisa maalumu kote nchini zinazotumia plasma kutibu majeraha.
-
Velayati: Ikiwa na Russia au bila ya Russia, Iran itaukwamisha ushoroba wa Marekani eneo la Qafqaz
Aug 09, 2025 23:48Ali Akbar Velayati, Mshauri mwandamizi wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itapinga kuanzishwa ushoroba wa usafirishaji na wa nishati unaodhibitiwa na Marekani nchini Armenia, jambo ambalo amesema litasababisha hatari kubwa kwa utulivu wa kanda hii.
-
Ayatullah Khamenei amteua Larijani kuwa mwakilishi wake katika Baraza Kuu la Usalama wa Taifa
Aug 07, 2025 22:48Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amemteua mwanasiasa mkongwe, Ali Larijani, kuwa mwakilishi wake katika Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC)
-
Iran yamnyonga gaidi wa kitakfiri wa Daesh aliyepatikana na hatia
Aug 06, 2025 09:03Mamlaka za Mahakama nchini Iran zimemnyonga mwanachama wa kundi la kigaidi na Kitakfiri la Daesh aliyepatikana na hatia ya kufanya mashambulizi ya kigaidi hapa nchini.
-
Ali Larijani ateuliwa Mkuu Mpya wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran
Aug 06, 2025 04:30Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemteua mwanasiasa mkongwe Ali Larijani kuwa Mkuu Mpya wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC).