-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran akutana na mawaziri wa Benin, Kodivaa
Oct 16, 2016 10:17Mawaziri wa mambo ya nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Ivory Coast wamekutana na kufanya mazungumzo mjini Tehran.
-
Jibu la Iran kwa taarifa ya Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi
Oct 16, 2016 03:34Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema chimbuko la mgogoro katika eneo la Mashariki ya Kati ni matokeo ya baadhi ya nchi kutaka ziwe na nguvu na mamlaka na uungaji mkono wao kwa makundi ya kigaidi na yenye misimamo ya kufurutu mpaka.
-
Iran yakaribisha hatua ya UNESCO kuhusiana na Msikiti wa Al-Aqsa
Oct 15, 2016 23:45Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekaribisha hatua ya Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) ya kuthibitisha haki ya wananchi wa Palestina kuhusiana na ardhi na matukufu yao.
-
Kiongozi: Ni marufuku kwa Serikali, Bunge, Mahakama, vikosi vya ulinzi, kuingilia uchaguzi Iran
Oct 15, 2016 12:28Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametumia haki yake aliyopewa na kifungu nambari 110 cha Katiba, kuwasilisha siasa kuu za uchaguzi baada ya kushauriana na Halmashauri ya Kuainisha Maslahi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Iran yaonya juu ya kuendelea kuuziwa silaha Saudia, Israel
Oct 15, 2016 04:43Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa ameonya kuhusu kuendelea kuuziwa silaha utawala wa kifalme wa Saudi Arabia na utawala wa Kizayuni wa Israel na kusisitiza kuwa hatua hiyo itakuwa na maafa makubwa katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Jeshi la Iran lanasa kundi linalotekeleza njama za kuibua farqa baina ya Waislamu
Oct 14, 2016 06:03Sambamba na jeshi la Iran kutangaza kuwatia mbaroni magaidi wakufurishaji waliokuwa wanapanga njama za kutekeleza hujuma za kigaidi katika maombolezo ya Tasua na Ashura za Imam Hussein (as), mjukuu wa Mtume (saw), Mwendesha Mashtaka Mkuu katika mji wa Zahedan, mkoa wa Sistan na Baluchestan, kusini mashariki mwa nchi ametangaza kutiwa mbaroni kundi la watu wenye siasa kali.
-
Iran: Tumewanasa magaidi 11 wakijiandaa kushambulia maombolezo
Oct 14, 2016 01:21Kamanda wa vikosi vya usalama nchini Iran ametangaza habari ya kutiwa mbaroni magaidi 11 katika mkoa wa Fars, kusini mwa nchi wakiwa na kilo 100 za mada za miripuko.
-
Russia: Tayari tumeikabidhi Iran mfumo wa makombora wa S 300, kwa mujibu wa mauziano yetu
Oct 14, 2016 01:18Afisa wa ngazi ya juu wa jeshi la Russia amesema kuwa, tayari nchi yake imeikabidhi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, mfumo kamili wa makombora wa S-300.
-
VIDEO + PICHA: Rais Rouhani alipozindua mfumo wa kisasa wa Iran wa kujilinda na makombora Bavar 373
Oct 13, 2016 12:45Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amezindua mfumo wa kisasa kabisa wa kujilinda na makombora uliotengenezwa na wataalamu wa Iran ambao una nguvu kuliko ule wa S300 wa Russia. Mfumo huu wa makombora wa Iran unaitwa Bavar-373
-
Iran yazima njama za magaidi wakati wa Ashura
Oct 13, 2016 04:27Vyombo vya usalama nchini Iran vimetibua njama ya kutekelezwa mashambulizi ya kigaidi hapa nchini wakati wa maombolezo ya Ashura ya kukumbuka tukio chungu la kuuawa Shahidi Imam Hussein AS, mjukuu wa Mtume Mtukufu SAW.