-
Uungaji mkono wa Marekani kwa makundi yanayotaka kujitenga ya Iran
Nov 25, 2022 23:01Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imelaani operesheni za kijeshi Iran dhidi ya makundi ya kigaidi ya Wakurdi wanaotaka kujitenga yaliyoko kaskazini mwa Iraq na imeitaka Tehran kusitisha mashambulizi hayo.
-
Al Sudani afanya mazungumzo na mrithi wa kiti cha ufalme wa Kuwait
Nov 23, 2022 22:54Waziri Mkuu wa Iraq amekutana na kufanya mazungumzo na mrithi wa kiti cha ufalme wa Kuwait na kusisitiza juu ya ulazima wa kuimarisha uhusiano kati ya nchi mbili.
-
Iraq yawatia nguvuni magaidi 15 wa Daesh
Nov 18, 2022 22:59Vikosi vya usalama vya Iraq vimewatia mbaroni magaidi 15 wa kundi la Daesh katika mikoa sita ya nchi hiyo.
-
Abdollahian: Iraq ina wajibu wa kuzuia vitisho dhidi ya Iran kutokea Kurdistan
Nov 15, 2022 04:08Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa mwito kwa jirani yake Iraq kuchukua hatua za kuzuia vitisho vinavyopangwa na kutekelezwa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu kutokea eneo lenye mamlaka ya ndani la Kurdistan, kaskazini mwa Iraq.
-
IRGC yashambulia tena ngome za magaidi Kurdistan ya Iraq
Nov 14, 2022 07:44Kwa mara nyingine, Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limeshambulia na kuharibu ngome za magaidi katika eneo lenye mamlaka ya ndani la Kurdistan, kaskazini mwa Iraq.
-
Mkwamo wa kisiasa wa Iraq wamalizika baada ya Bunge kupasisha serikali ya al-Sudani
Oct 28, 2022 07:13Bunge la Iraq limeipasisha serikali ya Waziri Mkuu Mohammad Shia al-Sudani baada ya kuipigia kura ya kuwa na imani nayo.
-
Iraq katika mchakato wa kuvuka mkwamo wa kisiasa wa mwaka mmoja
Oct 15, 2022 23:00Hatimaye bunge la Iraq limemchagua rais mpya wa nchi hiyo Abdul Latif Rashid ambapo rais huyo pia katika hatua yake ya awali amemteua Mohammed Shia al-Sudani kuwa Waziri Mkuu na kumpatia jukumu la kuunda serikali.
-
Rais wa Iran aipongeza Iraq kwa kuchagua rais mpya
Oct 14, 2022 04:26Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameipongeza serikali na wananchi wa Iraq, kufuatia kuchaguliwa na Bunge, Abdul Latif Rashid kuwa rais mpya wa nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Iran: Diplomasia haikukomesha uwepo wa magaidi Iraq, tumelazimika kuushughulikia kijeshi
Oct 12, 2022 23:47Ofisi ya uwakilishi wa kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa imemwandikia barua Rais wa Baraza la Usalama la umoja huo kubainisha hoja na sababu ya kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya makundi ya kigaidi yaliyoko nchini Iraq na kusisitiza kuwa diplomasia haikuweza kukomesha kuwepo kwa magaidi kaskazini ya nchi hiyo na ndio maana Iran imelazimika kutumia nguvu za kijeshi.
-
Amir-Abdollahian: Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq alikuwa amebeba salamu za Marekani kwa Iran
Sep 30, 2022 04:29Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema, katika kipindi cha miezi iliyopita baadhi ya mawaziri wa mambo ya nje wa nchi kadhaa wamekuwa wakifikisha jumbe za Marekani kwa Iran na kinyume chake, na akaongeza kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq, Fuad Hussein naye pia alikuwa amebeba ujumbe wa salamu za Marekani kwa Iran.