-
Magaidi wanne wakufurishaji watiwa nguvuni mkoani al Anbar, Iraq
Mar 05, 2022 02:55Vikosi vya usalama vya Iraq vimewatia nguvuni magaidi wanne wakufurishaji wa genge la Daesh (ISIS) katika operesheni waliyofanya katika mkoa wa al Anbar wa magharibi mwa nchi hiyo.
-
Baada ya kulipa gharama za kuivamia kijeshi Kuwait, Iraq yaondolewa kwenye Sura ya 7 ya UN
Feb 24, 2022 03:03Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq ametangaza kuwa nchi hiyo imeondolewa kwenye orodha ya Sura ya 7 ya Hati ya Umoja wa Mataifa.
-
Khatibzadeh: Iran inasubiri majibu ya Wamagharibi katika mazungumzo ya Vienna
Feb 14, 2022 10:58Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, hakuna mkwamo wowote katika mazungumzo ya Vienna na kilichopo ni kwamba hivi sasa Iran inasubiri majibu kutoka kwa nchi za Magharibi zinazoshiriki kwenye mazungumzo hayo.
-
Khazali: Wanamuqawama wa Iraq watajibu uchokozi mpya wa Uturuki
Feb 03, 2022 02:30Katibu Mkuu wa harakati ya Asa'ib Ahl al-Haq ambalo ni tawi la muungano wa makundi ya muqawama wa Hashd al-Sha’abi nchini Iraq amesisitiza kuwa, mrengo wa mapambano ya Kiislamu utatoa jibu mwafaka kwa uvamizi na chokochoko mpya za jeshi la Uturuki dhidi ya nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Watu wanane wameuawa na kujeruhiwa katika mashambulizi ya ndege za kivita za Uturuki kaskazini mwa Iraq
Feb 02, 2022 07:57Vyombo vya habari vimetangaza kuwa watu wasiopungua wanane wameuawa na kujeruhiwa katika mashambulizi ya ndege za kivita za Uturuki katika mji wa Sinjar kaskazini mwa Iraq.
-
Sauti ya mlipuko yasikika Baghdad mji mkuu wa Iraq
Jan 24, 2022 08:17Duru za habari zimearifu kuwa sauti ya mlipuko imesikika mapema leo magharibi mwa Baghdad mji mkuu wa Iraq.
-
Kutiwa nguvuni maafisa wa ngazi za juu wa upelelezi Iraq kwa kufanya ujasusi kwa maslahi ya Mossad
Jan 22, 2022 11:55Baadhi ya duru za Iraq zimetangaza kuwa Mahakama Kuu ya nchi hiyo juzi Alhamisi iliagiza kutiwa mbaroni maafisa wanne wa ngazi ya juu wa Idara ya Intelijinsia ya nchi hiyo kwa uhalifu wa kuasisi mtandao wa kijasusi kwa maslahi ya Shirika la Ujasusi la Israel na Kitengo cha Oparesheni Maalumu cha Mossad.
-
Barham Salih: Shambulio la Diyala linaonyesha kushindwa magaidi nchini Iraq
Jan 22, 2022 08:47Rais wa Iraq almesisitiza kuwa shambulio la kigaidi katika mkoa wa Diyala ni kitendo cha chuki kinacholenga usalama wa Iraq.
-
Walowezi wa Kizayuni wavamia tena msikiti mtakatifu wa al-Aqswa
Jan 11, 2022 02:40Makumi ya walowezi wa Kizayuni wameuvamia tena msikiti wa al-Aqswa huko Palestina na kuuvunjia heshima msikiti huo ambao ni kibla cha kwanza cha Waislamu.
-
Wanajeshi magaidi wa Marekani waiba makumi ya malori ya mafuta ya Syria
Jan 10, 2022 12:03Duru za kiusalama za Syria zimetangaza kuwa, muungano vamizi unaoongozwa na wanajeshi magaidi wa Marekani umeiba malori mengine 79 ya mafuta ya Syria na kuyaingiza nchini Iraq.